Biblia—Kitabu cha Wanadamu cha Kale Zaidi Kilicho cha Kisasa
1 Biblia ni kitabu ambacho kimesambazwa kwa wingi zaidi katika historia yote. Hakuna kitabu kingine ambacho kimetafsiriwa katika lugha nyingi sana. Kwa kuongezea, hakuna kikundi kinginecho chote ambacho kimekuwa na bidii kama Mashahidi wa Yehova katika kugawanya Biblia na kuitangaza peupe kuwa Neno la Mungu.
2 Kwa kuwa ni Neno la Mungu, twaweza kuwa na uhakika kwamba hilo hutoa majibu yafanyayo kazi kwa matatizo ya ki-sikuhizi. Nalo tengenezo la Yehova hutoa msaada wenye kutumika wa kupata majibu hayo katika vichapo pia na video. Hivyo basi twafurahi kutangaza kwamba chapa ya Kiingereza ya The Bible—Mankind’s Oldest Modern Book, ya pili kati ya video tatu inayoonyesha uvuvio wa Biblia, yaweza sasa kuagizwa kutoka kutaniko lako. Ni ya muda wa dakika 40.
3 Kama vile ile video ya kwanza ya mfululizo huu, hii ya pili pia yajenga uhakika katika Biblia kuwa uongozi wa kimungu. Inatumia mandhari zilizotolewa katika mabara ya Biblia na majumba ya hifadhi ulimwenguni ili zitusaidie tutambue jinsi Yehova Mungu amehifadhi Biblia kwa karne nyingi hadi siku yetu. Utaona vile usahihi wa Biblia umesitawishwa kujapokuwa kunakiliwa na kutafsiriwa kwa kurudiwarudiwa. Utaona jinsi kitabu hiki cha kimungu kimehifadhiwa wakati wa upinzani mkali hadi kugawanywa kwacho. Pia utaona ushuhuda uliopo wa jinsi Biblia imebadili maisha za watu kwa uzuri.
4 Video hii itakuwa yenye thamani kwa mazungumzo ya Biblia kwa familia na kwa makusudi mengine mengi yenye kutumika—kama tu ile ya kwanza. Tuna hakika kwamba Yehova atabariki utumizi wayo. Wale ambao hawajaiagiza wanaweza kufanya hivyo upesi kupitia idara ya fasihi katika kutaniko. Video The Bible—Accurate History, Reliable Prophecy na Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name bado zapatikana.