Habari Za Kitheokrasi
Kenya: Mkutano wa Halmashauri ya Uhusiano na Hospitali ulifanywa katika ofisi ya tawi Nairobi kutoka Aprili 10-14, 1994. Ndugu waliopokea mazoezi walikuja kutoka nchi karibu zote zilizo chini ya tawi pia kutoka India, Pakistan, na Sri Lanka. Wafunzi kutoka makao makuu ya Sosaiti Brooklyn walitoa mazoezi mazuri. Twatazamia kupokea manufaa ya mpango huu.
Mei 1, 1994 ilikuwa siku ya kuhitimu kwa wanafunzi 25 wa darasa la kwanza la Shule ya Mazoezi ya Kihuduma kwa Afrika Mashariki. Wahudhuriaji 294 walifurahia programu yenye kuchochea na wakawatakia wanafunzi mema wanapoenda kwenye migao yao katika nchi 6 za mashariki mwa Afrika.
Japani: Februari ulikuwa mwezi wenye baridi sana ukiwa na barafu nyingi. Hata hivyo, kilele kipya cha wahubiri 188,844 kilifikiwa. Pia kulikuwa na vilele vipya vya ziara za kurudia, mafunzo ya Biblia, na mapainia wa kawaida.