Habari za Kitheokrasi
◆ Kanada ilipita alama ya jumla ya wahubiri 100,000 wakati wa Aprili, ikiwa na kilele kipya cha wahubiri 100,368.
◆ Visiwa Cape Verde vilikuwa na kilele cha wahubiri 410 katika Aprili likiwa ongezeko la asilimia 19 zaidi ya wastani wa mwaka jana. Wahubiri wa kundi walikuwa na wastani wa saa 14.5, na kilele cha mafunzo ya Biblia 856 kiliripotiwa.
◆ Aprili ulikuwa mwezi wenye kutokeza katika Hondurasi. Walifikia vilele vipya katika wahubiri, mapainia, saa, magazeti, ziara za kurudia, na mafunzo ya Biblia. Pia makundi matatu zaidi yaliundwa. Wale wahubiri 5,706 waliongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani 9,614.
◆ Afrika Kusini ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 48,590 katika Aprili. Pia walikuwa na kilele chenye kutokeza cha mafunzo ya Biblia 49,967.
◆ Katika Tanzania 5,433 walihudhuria mfululizo wa makusanyiko ya mzunguko katika mwaka wa utumishi wa 1990 na 139 walibatizwa.