Habari Za Kitheokrasi
Chile: Kati ya wahubiri 42,778 walioripoti katika Aprili, 8,680 walikuwa mapainia. Kilele kipya cha mapainia wa kawaida 2,820 kilifikiwa. Jumla ya saa zilizoripotiwa kwa ajili ya Aprili ilikuwa 1,009,001.
Lesotho: Jumla ya wahubiri wenye kuripoti katika Aprili ilikuwa 1,895, ambalo lilikwa ongezeko la asilimia 19 zaidi ya wastani wa mwaka uliopita.
Ureno: Kilele kipya cha wahubiri 41,472 kilifikiwa katika Aprili. Kulikuwa na vilele vipya pia katika jumla ya saa, ziara za kurudia, na mafunzo ya Biblia.
Venezuela: Kazi yenye bidii ya wahubiri 62,074 wakati wa Aprili ilitokeza vilele vipya katika saa, ziara za kurudia, na mafunzo ya Biblia.
Hivi majuzi makutaniko yafuatayo yaliweka wakfu Majumba yao ya Ufalme:
Gitaru, Siaya na Limuru katika Kenya. Mbeya Mjini, Mbeya Isanga, Mbeya Sinsitila, na Kyela katika Tanzania. Makutaniko mengine yanapanga kuweka wakfu Majumba yao ya Ufalme hivi karibuni.