Sanduku La Swali
◼ Mambo yanapaswa kushughulikiwaje mwenye nyumba anaposisitiza kwamba Mashahidi wa Yehova wasifanye ziara zaidi nyumbani mwake?
Tunapokuta ishara mlangoni inayokataza kabisa ziara za namna ya kidini na hasa zinazotaja Mashahidi wa Yehova, itafaa kuheshimu matakwa ya mwenye nyumba na kuepuka kubisha mlango.
Wakati mwingine sisi hukuta ishara zenye kukataza wachuuzi au waombaji. Kwa kuwa tunafanya kazi ya kutoa msaada wa kidini, hilo kwa kweli halituhusu sisi. Ingefaa kubisha milango kama hiyo. Mwenye nyumba akipinga, twaweza kumweleza kwa busara ni kwa nini ishara kama hizo hazituhusu. Mwenye nyumba akieleza wazi kwamba kizuizi hicho chatia ndani Mashahidi wa Yehova, tutaheshimu matakwa yake.
Tunapohubiri eneo, mwenye nyumba anaweza kuwa na kukasirika kiwazi na asisitize sana kwamba tusirudi tena. Akikataa kusababu juu ya jambo hilo, twapaswa kufuata ombi hili. Maandishi ya tarehe iliyowekwa yapaswa kutiwa kwenye bahasha ya eneo ili kwamba wahubiri wanaohubiri eneo hilo wakati ujao waepuke kurudi kwenye nyumba hiyo.
Nyumba hizo hazipaswi kuepukwa hadi wakati usiojulikana. Wenye kuishi humo sasa huenda wakahama. Huenda tukapata mshiriki mwingine wa familia ambaye ataitikia vizuri. Kuna uwezekano pia wa kwamba mwenye nyumba ambaye tuliongea naye akawa na moyo uliobadilika na akawa mwenye kukubali zaidi turudi. Kwa hiyo baada ya muda fulani ulizo la busara lapaswa kuulizwa kuhusu wakazi hao ili kujua hisia zao za sasa.
Makutaniko yapatapo tatizo lililo juu faili ya eneo yapaswa kupitiwa mara moja kwa mwaka, kufanya orodha ya makao ambayo tumeshauriwa tusiende. Chini ya mwelekezo wa mwangalizi wa utumishi, wahubiri fulani wenye busara, wenye maarifa, wanaweza kupewa mgawo wa kutembelea makao haya. Inaweza kuelezwa kwamba tunazuru kujua kama mwenye nyumba yule yule bado anaishi humo. Mhubiri apaswa kuwa anafahamu habari iliyoko kwenye kitabu Kutoa Sababu, kurasa 15-24, yenye kichwa “Unavyoweza Kujibu Vikitokea Vizuia-Mazungumzo.” Ikiwa kuna itikio linalofaa, ziara za wakati ujao zaweza kufanywa kwa njia ya kawaida. Mwenye nyumba akiendelea kuwa mwenye kupinga, ziara zozote za kurudia zisifanywe hadi mwaka ujao. Baraza la wazee la mahali hapo wanaweza kuamua ikiwa hali za kisa fulani zaweza kufanya mambo yashughulikiwe kwa njia tofauti.