Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Jinsi ya Kumjibu Mtu Anayekataa Mazungumzo
Kwa Nini ni Muhimu: Wazia kwamba unajua kutakuwa na msiba wa asili. Watu watakufa ikiwa hawatakimbilia mahali salama. Unaenda kwa jirani yako kumpa tahadhari, lakini yeye anakatisha mazungumzo akisema ana shughuli nyingi. Kwa kweli, hutaacha kumsaidia! Watu wengi katika eneo letu wanatupinga, kwa kuwa hawatambui thamani ya ujumbe wetu wenye kuokoa uhai. Tunapowatembelea, huenda wakati huo wakawa na shughuli nyingi. (Mt. 24:37-39) Au labda wana maoni yasiyofaa kwa sababu wamesikia uvumi au maneno yasiyo ya kweli. (Mt. 11:18, 19) Huenda wakadhani kwamba hatuna tofauti na dini nyingine. (2 Pet. 2:1, 2) Ikiwa mwanzoni mwenye nyumba hapendezwi na ujumbe wetu, tusikate tamaa haraka.
Jaribu Dokezo Hili Kwa Mwezi Mzima:
Unapokutana na mtu anayekataa mazungumzo, baada ya kuondoka, zungumza na mwandamani wako jinsi ungeweza kumjibu kwa njia bora zaidi.