Sanduku La Swali
◼ Mwandishi apaswa kufanya nini painia wa kawaida ahamiapo kutaniko hilo?
Mwandishi apaswa kujulisha Sosaiti, akitumia nafasi iliyowekwa nyuma ya Ripoti ya Kutaniko (S-1-SW). Pia apaswa kuwasiliana upesi na mwandishi wa kutaniko la zamani la painia huyo na aombe kadi zote za Maandishi ya Mhubiri ya Kutaniko (S-21-SW) zilizo kwenye faili pamoja na barua ya kujulisha kutoka Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko.
Painia afanyapo uhamaji mkubwa, kwa kawaida yeye huwa na magumu fulani katika kutulia na kuanzisha kawaida nzuri ya utumishi. Painia huthamini wazee watoapo msaada wenye upendo kwake ili kuhama kwake kwenye kutaniko jipya kuwe bila matatizo ikiwezekana.
Kikumbusha: Mwandishi hutoa kadi za Kitambulisho cha Utumishi wa Painia (S-202-SW) tu kwa mapainia ambao wanahamia kutaniko kutoka nchi ileile. Mapainia wanaopoteza kadi yao, ambao wanabadilisha jina kwa sababu ya ndoa au talaka, au wanaohamia maeneo yanayoshughulikiwa na tawi jingine (kutia na wale wanaohama kutoka nchi nyingine iliyo Afrika mashariki) wapaswa kupokea kadi yao mpya kutoka kwa Sosaiti, si kwa mwandishi. Mwandishi au painia apaswa kuandikia Sosaiti, aeleze hali, na kuomba kadi mpya.