Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/94 uku. 1
  • Wajue Ndugu Zako Vizuri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wajue Ndugu Zako Vizuri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • “Iweni na Upendo Wenye Juhudi Nyingi Nyinyi kwa Nyinyi”
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Endelea Kukua Katika Upendo wa Kindugu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Pata Kuwajua Ndugu Zako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Watie Moyo Wanawake Wakristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 8/94 uku. 1

Wajue Ndugu Zako Vizuri

1 Uhusiano wetu na waabudu wenzetu watia ndani mengi zaidi ya kuhudhuria mikutano tu pamoja nao kwenye Jumba la Ufalme. Sisi ni wafanyi wa mapenzi ya Mungu, nako hutuleta katika uhusiano wa kiroho pamoja na Yesu. (Mk. 3:34, 35) Huo, nao, hutuleta kwenye uhusiano wa familia ya kiroho na wengine katika kutaniko la Kikristo, ndugu na dada zetu wa kiroho, ambao twaamuriwa kuwapenda. (Yn. 13:35) Hivyo, wale wanaoshirikiana na “watu wa nyumbani mwake Mungu” wanapaswa kujitahidi kujuana vizuri.—Efe. 2:19.

2 Wajue Ndugu Zako kwa Majina: Je, wajua majina ya ndugu na dada wote katika Funzo la Kitabu la Kutaniko lenu? Kwa kawaida kikundi huwa kidogo, ikifanya iwe rahisi zaidi kujua majina ya walio wengi, ikiwa si wote, wanaohudhuria. Ikiwa hata hujui majina yao, waweza kusema kwamba unawajua vizuri?

3 Vipi juu ya kuwajua wengine, kutia na watoto, wanaohudhuria mikutano katika Jumba la Ufalme? Huenda tukaelekea kushirikiana na kikundi kidogo tu cha marafiki. Ijapokuwa si vibaya kufurahia ushirika wa watu hususa, hatungetaka kuweka mipaka ya salamu zetu changamfu na mazungumzo yenye kujenga kwa wachache tu. Twapaswa ‘kupanuka,’ tukijitahidi kujua ndugu na dada zetu wote vizuri. (2 Kor. 6:11-13, NW) Hiyo bila shaka itatia ndani kuwajua kwa majina.

4 Akina ndugu wanaoongoza mikutano ya kutaniko wapaswa kujaribu kujua majina ya wote wanaohudhuria. Kuwaita kila mmoja kwa majina kutoka jukwaani huwafanya wahisi kwamba maelezo yao yanathaminiwa, na wakati uleule, husaidia wengine wajue majina yao. Bila shaka, sikuzote kutakuwepo na wapya au wageni miongoni mwa wasikilizaji, ikifanya iwe vigumu kwa mtu yeyote kujua kila jina. Ingawa hivyo, jitihada yenye kuendelea ya moyo mnyoofu ni yenye kutia moyo kwa wengine nayo hurejezea kupendezwa kibinafsi kikweli.—Rum. 1:11, 12.

5 Chukua Hatua ya Kwanza Kufahamu Vizuri: Waangalizi wasafirio kwa kawaida huweza kufahamu idadi kubwa ya ndugu na dada. Wao hufanyaje hivyo? Kwa njia tatu za msingi: (1) Wao huhubiri nao kwa kawaida katika utumishi wa shambani; (2) hali zao zinaporuhusu, wao hukubali mialiko ya kuwatembelea nyumbani mwao; na (3) wao huchukua hatua ya kwanza kuwasalimu watu wazima na watoto kwenye mikutano.

6 Je, waweza kuona njia za kupanuka katika mashirika yako na kuwajua ndugu zako vizuri? Kwa hakika twaweza kuwaalika wengine wajiunge nasi katika utumishi wa shambani. Kwenda nyumba kwa nyumba, kufanya ziara za kurudia, kwenda kwa mafunzo ya Biblia, au kutoa ushahidi wa barabarani na magazeti ni njia zilizo bora zaidi za kufahamu vizuri. Pia ni vizuri kuwakaribisha wengine watembelee makao yako, labda mkishiriki mlo au viburudisho mara kwa mara. Kuchukua hatua ya kwanza kuwafikia wapya au wale wanaoelekea kuwa na haya si kwamba huwajenga sana kiroho tu bali pia huwaletea dhawabu kubwa.—Mdo. 20:35; 1 The. 5:11.

7 Paulo aliwajua ndugu zake vizuri. Kwa kuwarejezea wengi wao binafsi mara nyingi kwa majina katika barua zake ni uthibitisho wa kupendezwa kwake nao kusiko kwa choyo na upendo wake wa kweli kwao. (1 The. 2:17; 2 Tim. 4:19, 20) Jitihada zetu za kujua ndugu zetu vizuri zitamaanisha baraka kwetu sote.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki