Hangaikia Kutoa Magazeti Wakati wa Oktoba
1 Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yana ujumbe wenye kufariji na kutia moyo wa habari njema za milele. Kuwa mwenye kuhangaikia kutoa magazeti kwatia kuchukua wakati kuyasoma kwa uangalifu na kufikiria jinsi makala hizo zaweza kuvutia watu katika eneo letu.
2 Kwanza, fahamu makala zinazoonyeshwa kwenye jalada. Vielezi vya jalada vyenyewe vitafanya magazeti yachukuliwe. Chagua makala ambazo unahisi zitawavutia watu kwenye eneo lenu. Je, watu ni wa imani ya dini moja? Hangaikio lao kubwa ni nini? Ukiwa na mawazo hayo akilini, unapaswa kuweza kutayarisha utoaji wenye matokeo. Angalia yale yanayotolewa hapa chini.
3 Ikiwa unatoa “Mnara wa Mlinzi” la Septemba 1, unaweza kukazia ile makala “Sayansi, Dini na Jitihada ya Kutafuta Kweli.” Unaweza kusema:
◼ “Unaweza kupata Biblia katika karibu kila nyumba kwenye jamii yetu. Wengi walio nayo wanahisi kwamba ina kitu fulani kilicho na thamani ya pekee.” Kisha unaweza kuuliza swali la moja kwa moja, kama vile: “Unafikiri ni nini huifanya Biblia iwe isiyo na kifani?” au, “Unafikiri ni nini kitakachosaidia watu wengi zaidi wanufaike na Biblia?” Ukifuatia itikio la mwenye nyumba, unaweza kuendelea na maelezo yanayofaa, kama vile: “Kuna ushuhuda uliojaa wa kuthibitisha kwamba Biblia imepuliziwa na Mungu na ni mwongozo wenye kutegemeka kwetu. Ina ujuzi uwezao kutuongoza kwenye uhai wa milele. [Soma Yohana 17:3.] Watu wengi wanaiheshimu lakini wao huhisi inapingana na sayansi na ujuzi wa karne ya 20. Makala hii kwenye Mnara wa Mlinzi yakusudia kusuluhisha yale watu fulani wanafikiri ni tofauti za masimulizi ya uumbaji.” Kisha geukia vielelezo vilivyotolewa chini ya kichwa kidogo kwenye ukurasa 6. Malizia na fungu la mwisho kwenye ukurasa 7 na utoe andikisho.
4 Ukitumia “Mnara wa Mlinzi” la Septemba 15, unaweza kupendelea mfikio sahili kama huu:
◼ “Tunaongea na watu ambao wanapendezwa na jinsi tunavyoweza kukabiliana na matatizo ya maisha ya familia. Sisi sote hujaribu kufanya tuwezavyo, lakini ikiwa kuna jambo ambalo twaweza kufanya ili tuwe na mafanikio mengi, tunapendezwa, sivyo? Kwa sababu ya kutokamilika kwetu sote katika familia twaweza kufikiria maneno haya kwenye Wakolosai 3:12-15.” Baada ya kusoma na kuzungumzia mistari hii waweza kuelekeza uangalifu kwa manufaa za kusamehe kama ionyeshwavyo kwenye ukurasa wa 7 wa makala hiyo. Onyesha kwamba hiki ni kiolezo tu cha habari yenye kutumika inayopatikana katika Mnara wa Mlinzi na kwamba andikisho kwa hakika utanufaisha familia nzima.
5 Jitahidi kutoa andikisho katika kila mlango na kwenye kila pindi. Ndugu mmoja katika Mumias, alifuata dokezo la kutoa maandikisho mahali pake pa kazi, alifanikiwa kupata maandikisho 120 kwa muda wa miezi miwili. Jambo hili lilitokeza mafunzo ya Biblia nyumbani watano na watatu kati yao wanafanya maendeleo mazuri sana. Kwa hiyo kwa kuwa na fikira chanya tutahangaikia kutoa magazeti wakati wa Oktoba tukitoa andikisho katika kila pindi.