Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/95 uku. 4
  • Kutanguliza kwa Matokeo Kitabu Kuishi Milele

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutanguliza kwa Matokeo Kitabu Kuishi Milele
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Matangulizi ya Kuchochea Kupendezwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Utoaji Mbalimbali Ulio Rahisi na Wenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Fuatia Kupendezwa Ulikopata
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Sitawisha Kupendezwa Katika Kitabu Kuishi Milele
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 2/95 uku. 4

Kutanguliza kwa Matokeo Kitabu Kuishi Milele

1 Yesu alikuwa mwenye ustadi katika utumizi wake wa matangulizi. Yeye alijua yale ya kusema ili kuamsha kupendezwa. Kwenye pindi moja alianzisha mazungumzo pamoja na mwanamke Msamaria kwa kumwomba tu maji ya kunywa. Hilo lilinasa uangalifu wake mara hiyo kwa sababu ‘Wayahudi hawakuchangamana na Wasamaria.’ Hatimaye mazungumzo yaliyofuata yalimsaidia yeye na wengine wengi wawe waamini. (Yn. 4:7-9, 41) Sisi twaweza kujifunza kutokana na kielelezo chake.

2 Utayarishapo kutoa kitabu Kuishi Milele, jiulize mwenyewe, ‘Ni nini mambo yanayohangaisha watu kwa sasa katika eneo letu? Ni nini kitakachomvutia tineja, mtu mwenye umri mkubwa zaidi, mume, au mke?’ Ungeweza kutayarisha utangulizi zaidi ya mmoja na kupanga kutumia ule unaofikiri waifaa hali zaidi.

3 Kwa kuwa kuzorota kwa maisha ya familia kwahangaisha wengi, waweza kusema hivi:

◼ “Mibano ya kila siku ya maisha imewekea familia mikazo mikubwa leo. Wanaweza kupata msaada wapi? [Ruhusu jibu.] Biblia yaweza kuwa msaada halisi kwetu. [Soma 2 Timotheo 3:16, 17.] Maandiko hutoa miongozo yenye manufaa yawezayo kusaidia familia ziokoke. Ona yasemwayo katika fungu la 3 kwenye ukurasa 238 wa kichapo, Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.” Soma fungu la 3, na utoe toleo.

4 Ikiwa unatumia habari fulani ya mahali penu, waweza kusema hivi:

◼ “Je, ulisikia ripoti ya habari juu ya [taja jambo linalohangaisha mahali penu]? Wewe ulionaje jambo hilo? [Ruhusu jibu.] Lakufanya ujiulize ulimwengu huu unaelekea wapi, sivyo? Biblia ilitabiri mambo kama haya kuwa uthibitisho wa kwamba tunaishi katika siku za mwisho.” Kisha zungumzia habari iliyo katika kitabu Kuishi Milele, kurasa 150-153.

5 Wengi wanahangaishwa na tatizo la uhalifu linaloongezeka. Ungeweza kutumia utangulizi wa kwanza chini ya kichwa “Uhalifu/Kutopatwa na Madhara” kwenye ukurasa 13 wa kitabu “Kutoa Sababu”:

◼ “Tunazungumza na watu juu ya ulinzi wa kibinafsi. Kuna uhalifu mwingi katika ujirani wetu, nao unaathiri maisha zetu. Unafikiri ni nini kingehitaji kufanywa ili watu kama wewe na mimi tuhisi tukiwa salama barabarani usiku?” Waweza kusoma Zaburi 37:10, 11 na kuonyesha baraka ambazo Ufalme wa Mungu utaleta, kwa kutumia kurasa 156-158 za kitabu Kuishi Milele.

6 Ikiwa wapendelea mfikio ulio rahisi zaidi, waweza kutumia utangulizi unaofanana na ule unaopatikana kwenye ukurasa 14 katika kitabu “Kutoa Sababu”:

◼ “Tunawatia moyo jirani zetu wafikirie ule wakati ujao mtukufu ambao Biblia hututolea. [Soma Ufunuo 21:3, 4.] Je, hili lasikika likiwa zuri kwako? [Ruhusu jibu.] Sura ya 19 ya kichapo hiki yakazia baraka nyinginezo ambazo wanadamu watiifu watakuwa nazo chini ya Ufalme wa Mungu.” Kisha, toa kitabu Kuishi Milele.

7 Kutayarisha utangulizi wenye matokeo kwaweza kukusaidia ufikie wale wenye njaa ya kupata uadilifu.—Mt. 5:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki