Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/95 uku. 4
  • Saidia Wengine “Kuyashika Yaliyoandikwa”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Saidia Wengine “Kuyashika Yaliyoandikwa”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Kupiga Mbiu ya ‘Maneno ya Unabii’
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Wasaidie Waelewe
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Ufunuo—Ufunguo wa Furaha ya Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 3/95 uku. 4

Saidia Wengine “Kuyashika Yaliyoandikwa”

1 Hakutoshi ‘kusikia’ maneno ya unabii mwingi katika kitabu cha Ufunuo. Ili kunufaika kikamili, ni lazima mtu “kuyashika” yaliyoandikwa. (Ufu. 1:3) Kuangusha fasihi ni hatua ya kwanza tu kuelekea kufanya wanafunzi. Mara tupatapo wenye kupendezwa walio na nia ya kusikia, twapaswa kurudi upesi ili kuwasaidia kujifunza zaidi. Twaweza kuongea juu ya nini kwenye ziara yetu ya kurudia?

2 Ikiwa ulisema juu ya wale wapanda-farasi wanne wa ufananisho kwenye ziara yako ya kwanza, waweza kuanza mazungumzo yako kwa njia hii:

◼ “Wakati uliopita tuliongea juu ya kitabu cha Ufunuo na jinsi unabii wacho mwingi unavyotimizwa leo katika matukio ya ulimwengu. Ufunuo sura ya 6 ilitabiri uendeshaji wa wale wapanda-farasi wanne wa ufananisho, ambao ungetokeza ujeuri na msononeko mwingi duniani. Tumeona hayo yakitendeka machoni petu wenyewe. Wengi hutaka kujua wakati msononeko huu utakapoisha ili tuweze kufurahia maisha katika ulimwengu wenye amani. Maoni yako ni nini? [Ruhusu itikio.] Wanafunzi wa Yesu walipendezwa na jibu kwa swali hilo.” Soma Mathayo 24:3, ambapo swali hilo lilitokezwa, kisha mstari 34, ambapo Yesu alitoa jibu. Ungeweza kueleza zaidi juu ya siku za mwisho.

3 Ikiwa ulizungumzia Ufalme wa Mungu kwenye ziara ya kwanza, huenda ukaamua kuendelea kwa kuuliza swali hili:

◼ “Kwa maoni yako, je, wanadamu waweza wakati wowote kutosheleza mahitaji yote ya wanadamu? [Ruhusu itikio. Soma Yeremia 10:23.] Kama vile uwezavyo kuona, Mungu hakukusudia kwamba mwanadamu aelekeze mambo yake mwenyewe. Majaribio kufanya hivyo bila msaada wa Mungu ndicho kisababishi cha mengi ya matatizo yetu. Ufalme wa Mungu ndio serikali pekee iwezayo kuandaa tunachohitaji.” Fungua ukurasa 330 katika kitabu Kutoa Sababu, na uzungumzie maandiko yaliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza. Endelea na mazungumzo kwa kueleza kwa nini sisi twaweza kuweka tumaini letu lote katika Mungu.

4 Huenda ukataka kujaribu hili kuanzisha mazungumzo ya Kimaandiko:

◼ Onyesha kielezi kwenye ukurasa 302 wa kitabu Upeo wa Ufunuo, na ueleze hivi: “Wanadamu watafurahia hali hizi wakati mapenzi ya Mungu yanapofanywa duniani kama huko mbinguni. Hata hivyo, wengine wahofu kwamba hali mbaya zitarudi tena. Hiyo haitawezekana kwa sababu waovu wote watafutiliwa mbali.” Soma Zaburi 37:10, 11. Mkaribishe mwenye nyumba atumie kwa faida yake programu yetu ya funzo la Biblia ili ajifunze zaidi.

5 Ikiwa uliacha trakti “Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani,” elekeza kwenye kielezi kwenye upande wa mbele kisha usome fungu 1 chini ya kichwa “Uzima Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu.” Kisha useme:

◼ “Ikiwa twataka kuishi katika ulimwengu huo, kuna jambo la maana ambalo ni lazima tufanye.” Soma fungu la mwisho, na utoe kitabu Upeo wa Ufunuo.

6 Kwa kuwa kusudi letu ni kuanzisha mafunzo ya Biblia, twahitaji kufanya ziara za kurudia zenye matokeo. Ratibu wakati kwa ajili yazo, na utayarishe vizuri. Kwa njia hiyo twaweza kwa kweli kusaidia watu wenye mioyo ya haki.—Ufu. 22:6, 7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki