‘Endeleeni Kuongezeka Katika Ujuzi Sahihi’
Ujuzi sahihi wa Mungu huongoza kwenye uhai udumuo milele. (Yn. 17:3, NW) Tunapaswa kufanya yote tuwezayo ili kuongeza ujuzi sahihi kuhusu Yehova. (Kol. 1:9, 10) Kuanzia Aprili 29, tutakuwa tukisoma kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko. Uelewevu wetu wa Neno la Mungu utaongezwa na pia tutatayarishwa vizuri kufundisha wengine. Wewe na familia yako mtabarikiwa ikiwa mtatayarisha mapema, kuhudhuria na kushiriki kila juma, na kutumia yale mnayojifunza katika huduma.