Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/96 uku. 3
  • Je, Una Shughuli Nyingi Mno?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Una Shughuli Nyingi Mno?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Zinazolingana
  • “Acheni Sisi Pia Tuvue Kila Uzito”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Jinsi ya Kukomboa Wakati
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Mengi ya Kufanya Sikuzote
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Je! Waweza Kuwa Na Furaha Ukiwa Na Mengi Ya Kufanya?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 5/96 uku. 3

Je, Una Shughuli Nyingi Mno?

1 Paulo alihimiza kwamba ‘tuzidi kutenda kazi ya Bwana sikuzote.’ (1 Kor. 15:58) Twasihiwa tudumishe kawaida ya kila siku ya funzo la kibinafsi, kushiriki katika huduma kwa ukawaida, kuhudhuria mikutano kwa uaminifu, na kutunza migawo ya kutaniko kwa bidii. Kuongezea hayo, lazima tusaidie wengine wanaohitaji msaada wetu. Tukiwa na mengi zaidi ya kufanya, wakati mwingine huenda tukahisi tumelemewa, tukifikiria kwamba tunapaswa kutafuta njia za kupunguza kazi zetu.

2 Kuna hali ambazo huenda zikafanya iwe jambo la hekima na lenye kufikiri kuzuri kuondoa utendaji kadhaa au kupunguza kiwango chao. Watu wengine huhisi kwamba wanatazamiwa kufanya kila kitu ambacho wanaombwa na wengine. Ukosefu wa usawaziko katika jambo hili waweza kutokeza msongo na mkazo uwezao kuwa wenye kuangamiza hatimaye.

3 Uwe Mwenye Usawaziko: Ufunguo wa usawaziko uko kwenye shauri la Paulo la ‘kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi.’ (Flp. 1:10, NW) Hilo lamaanisha kwamba tukazie mambo yaliyo na umuhimu na, wakati na hali ziruhusupo, tuangalie mambo mengine yaliyo na umaana mdogo. Wajibu wa familia kwa hakika ni wa kwanza miongoni mwa mambo hayo yaliyo muhimu. Madaraka fulani ya kimwili lazima yashughulikiwe. Hata hivyo, Yesu alifundisha kwamba kipaumbele chetu chapaswa kutegemea kanuni ya kwamba twatafuta Ufalme kwanza. Lazima kwanza tufanye mambo ambayo yataturuhusu kutimiza wakfu wetu kwa Yehova.—Mt. 5:3; 6:33.

4 Tukiwa na jambo hilo akilini, tutahakikisha kwamba twaondoa kwenye ratiba yetu yenye shughuli nyingi ufuatiaji wowote wa kibinafsi usio wa lazima, utendaji mwingi sana wa tafrija, na ahadi zisizo za lazima kwa wengine. Katika kupangia utendaji wetu wa kila juma, tutaweka wakati kando kwa funzo la kibinafsi lifaalo, ushiriki wa kutosha katika utumishi, uhudhuriaji wa mikutano, na mambo mengine yoyote yahusianayo na ibada yetu. Wakati uliobaki waweza kugawanywa kwa ufuatiaji mwingine, ikitegemea ufuatiaji huo mbalimbali wachangia vipi kufikia miradi yetu ya msingi ya kuwa Wakristo wenye usawaziko wanaoweka Ufalme kwanza.

5 Hata tukifanya hivyo, huenda tukahisi mzigo wetu ni wenye kulemea. Ikiwa ndivyo, twahitaji kuitikia mwaliko wa Yesu: “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.” (Mt. 11:28) Pia, mtegemee Yehova, “[ambaye] siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu” naye humpa aliyechoka nguvu. Yeye aahidi kwamba hataruhusu mwadilifu apepesuke. (Zab. 55:22; 68:19; Isa. 40:29) Twaweza kuwa na uhakika kwamba sala zetu zitajibiwa, ikifanya iwezekane kwetu kuvumilia katika maisha yenye matokeo ya utendaji wa kitheokrasi.

6 Huku tukiwa na uhakika juu ya kuendelea kuwa wenye shughuli katika kufuatia masilahi yafaayo ya Ufalme, twaweza kuwa na shangwe katika kujua kwamba kazi yetu si bure katika Bwana.—1 Kor. 15:58.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki