Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 5/15 kur. 28-31
  • Je! Waweza Kuwa Na Furaha Ukiwa Na Mengi Ya Kufanya?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Waweza Kuwa Na Furaha Ukiwa Na Mengi Ya Kufanya?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kufaulu Kunaleta Furaha
  • Uwe Mwenye Kusawazika
  • Njia Zenye Kutumika za Kudumisha Usawaziko
  • Tumia Uamuzi Mzuri
  • Je, Wewe ni Painia Mwenye Usawaziko?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Je, Una Shughuli Nyingi Mno?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Ishi Maisha Yenye Usawaziko, Yaliyo Sahili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Hekima ya Kutuongoza Maishani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 5/15 kur. 28-31

Je! Waweza Kuwa Na Furaha Ukiwa Na Mengi Ya Kufanya?

WENGI wetu huwa na maisha yenye shughuli sana, mara nyingi ya mwendo wa mbio mbio. Mikazo yenye kukakamiza ya maisha ya ki-siku-hizi hutuhitaji tujitahidi daima ili tuweze kudumisha mwendo ulio sawa. Ni lazima waume na akina baba wapatane na wajibu wa familia zao, ya waajiri wao, na wengine. Ni lazima wake na akina mama watunze mahitaji ya nyumbani ya familia zao na mara nyingi wanapaswa kufanya kazi ya kimwili. Hata vijana wako chini ya mkazo wa kufululiza wajibu fulani wa kifamilia huku wakipata elimu ambayo itawatayarisha kwa daraka lenye matokeo katika jamii.

Lakini vipi juu ya wengine wetu ambao wameweka maisha zao wakfu kwa Yehova Mungu na ni Mashahidi wake wenye kubatizwa? Kuongezea hayo matakwa mengi yote yanayotakiwa kwetu, tuna himizo hili la mtume Paulo: “Ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.” (1 Wakorintho 15:58) Naam, madaraka mengi yaliyoongezeka ni sehemu ya matakwa ya ibada ya kweli. Tunaweza kutimizaje wajibu huo wote na kuwa na amani ya akili na mtazamo wenye furaha?

Kufaulu Kunaleta Furaha

Furaha—kuhisi hali njema au kuridhika—inahusiana kwa karibu na kufanikiwa katika kushughulika na madaraka ya maisha. Ikiwa tunaweza kutimiza wajibu wetu wa kila siku katika njia ya akili inayofaa, kufanya mambo bila kuchelewa na katika njia ya utaratibu, kufaulu na kuridhika. Hivyo ndivyo kunapaswa kuwa, na tokeo huchangia furaha yetu.

Yehova Mungu hakukusudia kamwe kwamba kushughulikia kwetu madaraka kuwe taabu yenye kulemea. Bali, sikuzote imekuwa tamaa yake kwamba ‘tufurahie na kuona mema kwa kazi yetu yote.’ (Mhubiri 3:12, 13, NW) Tunapofurahi katika kazi yetu, kwa kawaida tunakuwa na matokeo. Tunapokea maagizo kwa urahisi, na tunapatana na wengine kwa amani. Kwa upande mwingine, tusipokuwa na furaha, kazi yetu yaelekea kuwa ya uchovu—mkokoto usiobadilika, wenye kuchosha, hata wenye kulemeza maoni ya moyoni. Hiyo yaongoza kwenye tabia za kazi zisizo na matokeo na hali ya akilini isiyofaa. Maisha yawa ya kung’ang’ana kila siku tunapojaribu kutimiza matakwa yote yanayotakiwa kwetu. Hata hivyo, ikiwa tunaweza kupata njia ya kubaki kuwa wenye furaha katika yale tunayoyafanya, tunaelekea zaidi kupata njia ya maisha inayothawabisha na yenye kutimiliza.

Uwe Mwenye Kusawazika

Ikiwa tutakuwa wenye furaha ingawa tuna mengi ya kufanya, tunahitaji kuwa wenye kusawazika. Kusawazika ni nini? Ni “uthabiti wa kiakili na wa maoni ya moyoni.” Mtu aliyesawazika hujitahidi kuwa mwenye utaratibu katika utendaji wake. Yeye hupanga mbeleni, huepuka kuahirisha-ahirisha mambo, na ni mwenye kiasi katika mazoea. Yeye huonyesha kujidhibiti katika chakula, vinywaji, tafrija, shughuli za kujifurahisha, na kujitumbuiza. Kwa kweli, yeye huonyesha ‘kujidhibiti katika yote”!—1 Wakorintho 9:24-27, NW; linganisha Tito 2:2.

Sala ina sehemu muhimu katika kudumisha usawaziko wa Kikristo. Mtumishi wa Yehova aweza kusali kwa ajili ya roho takatifu ya Mungu na kwa ajili ya msaada wa Baba yake wa kimbingu katika kukuza matunda yayo, kutia na kujidhibiti. (Luka 11:13; Wagalatia 5:22, 23) Mkristo hasa apaswa kumtegemea Mungu katika sala anapopatwa na majaribu ambayo yatisha kusumbua usawaziko wake. “Umkabidhi BWANA [Yehova, NW] njia yako, pia umtumaini, naye atafanya,” akasema mtunga zaburi Daudi. (Zaburi 37:5) Huenda nyakati nyingine tukahitaji kusali alivyofanya Daudi alipoomba hivi: “Ee Mungu, unijilie kwa haraka. Ndiwe msaada wangu na mwokozi [Mwandalizi wa wokovu, NW] wangu, Ee BWANA [Yehova, NW], usikawie.” (Zaburi 70:5) Usisahau kamwe kwamba kwa sala inawezekana kudumisha usawaziko na kuonea shangwe ‘amani ya Mungu, ipitayo akili zote, inayohifadhi mioyo yetu na nia zetu.’—Wafilipi 4:6, 7.

Kwa sababu anamtegemea Yehova na kuonea shangwe amani ya Mungu, Mkristo mwenye kusawazika ni timamu katika akili. (Tito 2:11, 12) Hii hukuja kutokana na kuwa na ufahamu mzuri wa kanuni za Biblia na kwa kuzitumia maishani mwake. Mtu kama huyo si mnafiki, wala si mwenye haraka kuamua mambo. Kuwa mwepesi kukubali maoni ya wengine humzuia kuwa mwenye kushikilia kauli yake tu au kuwa mshupavu. Yeye hudumisha maoni ya kiasi juu yake mwenyewe na juu ya uwezo wake na hii humwezesha kushirikiana na wengine. (Mika 6:8) Kwa kupendeza, tabia ambazo humsaidia mtu asawazike ni zile pia zilizo miongoni mwa sifa zinazotakiwa kwa wale ambao wamewekwa kutumika wakiwa waangalizi katika kundi la Kikristo.—1 Timotheo 3:2, 3.

Tunaweza kuongezea sana kwenye furaha yetu kwa kujitahidi kuwa wenye kusawazika zaidi katika utendaji wetu wa kila siku. Kwa kuonyesha sifa zinazohusika na usawaziko mzuri, tunaweza kufanya mambo yanayohitajika bila mkazo wa kimwili au wa maoni ya moyoni. Mtindo-maisha wetu utaonyesha uthabiti mwingi zaidi, na tutatimiza mambo mengi zaidi. Wengine wataona ushirika wetu kuwa wenye kupendeza zaidi, nasi tutaona uradhi na shangwe nyingi zaidi. Lakini baadhi ya njia zenye kutumika za kudumisha usawaziko ni zipi?

Njia Zenye Kutumika za Kudumisha Usawaziko

Ili kudumisha usawaziko, tunapaswa kujaribu kuwa wepesi na wenye utaratibu katika kushughulikia mambo yetu ya kibinafsi. Tunahitaji kupanga mbeleni, kushughulika na mambo katika njia yenye utaratibu na yenye mpango. Wale wasio na mipango mizuri ya kibinafsi na wanaoelekea kuahirisha-ahirisha mambo hutatanisha maisha yao kwa kuongeza viwango vya mikazo na wasiwasi. Kufanikiwa katika jambo hili maishani kutatusaidia kuona kwamba tunaweza kudhibiti mambo badala ya kuona kwamba sisi ni watu hoi wanaowezwa na hali.

Hatupaswi kujaribu kufanya kila kitu peke yetu. Wale wasiotaka kukubali msaada kutoka kwa wengine mara nyingi hulipa bei kubwa sana kwa kuishiwa nguvu na kufadhaika. Kuna kazi mbalimbali ambazo zingeweza kushughulikiwa na wengine. Kwa hiyo, ni jambo la hekima kutumia uwezo mbalimbali wa wale ambao wanataka kusaidia. Zaidi ya kupunguza kazi yetu wenyewe, hiyo huenda ikawatia moyo wale ambao wanatamani kutukaribia zaidi.

Si jambo la hekima kujilinganisha na wale ambao huenda wakaweza kufanya zaidi. Kujaribu kuwa kama wale ambao wanaonekana wanatimiza zaidi ya vile tunavyoweza kunavunja moyo, kunatufanya tujione kuwa wadogo na wasiostahili. Kufikiri huko kunaharibu, kunadhoofisha uthabiti na uhakika wetu wa kibinafsi. “Kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe,” akaandika Paulo, “ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa [kulinganishwa na, NW] mwenzake.” (Wagalatia 6:4) Kumbuka kwamba mfanya kazi ambaye anathaminiwa sana ni yule ambaye anafuata maagizo, aliye thabiti na mwenye kutegemeka, na afanyaye kazi ya aina nzuri. Tukiwa hivyo, utumishi wetu mbalimbali utathaminiwa na kutakiwa kwa wingi.—Mithali 22:29.

Tunahitaji kutunza vizuri afya yetu. Hiyo ni moja ya mali zetu zenye thamani kubwa sana, kwa kuwa bila hiyo tungeweza kufanya kidogo sana. Hivyo, tunapaswa kujaribu kudumisha ulaji wenye afya kwa kula chakula kinacholisha mwili. Tunapaswa kupata pumziko tunalohitaji, kwenda kulala usiku katika saa inayofaa. Tunapochoka sana au kusikia kama tunapatwa na ugonjwa, hatupaswi kuendelea kujisukuma; huenda tukalipa bei kubwa.

Ni muhimu kujilinda dhidi ya kustawisha roho ya kulalamika. Tukijiachilia tuwe tukifikiri-fikiri mambo hasi, tunaweza kupata jambo baya katika kila kitu au kila mtu. Hiyo hakika ni njia moja ya kutunyang’anya sisi wenyewe na wengine shangwe. Badala ya kupiga porojo au kulalamika juu ya jambo ambalo tunaona si sawa, tunapaswa kuwajulisha wale ambao wana daraka la kushughulikia jambo hilo na kuwaacha wasahihishe mambo. (Linganisha 1 Wakorintho 1:10-12.) Tuna hekima tukidumisha mtazamo chanya, sikuzote tukitafuta na kutarajia kupata mazuri katika wengine na katika matukio yanayofanyiza maisha yetu.—Linganisha Yuda 3, 4, 16.

Katika kupanga utendaji wetu, tunapaswa kukumbuka kwamba mwendo wa haraka haraka huenda ukatimiza mambo mengi ajabu, lakini mara nyingi hauwezi kudumishwa kwa muda mrefu. Kujibidiisha daima kupita kiasi hakusababishi tu kuishiwa nguvu bali pia kunaweza kuleta kuvunjika moyo ambako kwaweza kudhoofisha azimio letu la kuendelea. Hivyo, acheni tuweke mwendo ambao tunaweza kudumisha kwa wakati usio dhahiri. Kwa mfano, ni vizuri kufanyiza ratiba yenye kutumika ya kushiriki kwa kawaida katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba na sehemu nyinginezo za huduma ya Kikristo. Tunahitaji kuruhusu wakati wa kupumzika na tafrija yenye kujenga. Na tutaona kuna manufaa kuongea na watu wa umri mkubwa zaidi ambao wana miongo ya ujuzi, kwa kuwa huenda ikawa wamejifunza jinsi ya kufanya mambo yanayohitajiwa bila kujichosha kimwili au katika maoni ya moyoni.

Tumia Uamuzi Mzuri

Inafaa kuona wajibu na tamaa ya kutimiza madaraka yetu tuliyowekewa, kutia na yale yaliyo katika kundi la watu wa Yehova. Yehova hupendezwa na wafanya kazi wenye bidii, wanaotegemeka. (Linganisha Mathayo 25:21; Tito 2:11-14.) Lakini Maandiko yanahimiza hivi: “Shika hekima kamili na busara.” (Mithali 3:21) Matumizi ya hekima ya Kibiblia yatatunufaisha, nasi tunahitaji kutumia busara na uamuzi mzuri, kufanya mipango yenye uangalifu na sikuzote kufanya mambo kiasi cha uwezo wetu.

Himizo la kuwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana lazima lisawazishwe na onyo linalopendekezwa kwenye Mhubiri 9:4. Hapo tunasoma hivi: “Afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa.” Naam, mbwa aliye hai, ingawa anadharauliwa na wengi, ni afadhali kuliko simba aliyekufa, mnyama ambaye watu wengine humwona kuwa wa kifalme. Tukizoea usawaziko na kutunza afya yetu inavyofaa, tutaishi na kuweza kuendelea kufanya mambo. Wafu hawana ushirika zaidi katika utendaji wowote. Uamuzi mzuri unaweza kutusaidia kupata usawaziko mzuri ambao utaturuhusu kufanya mambo yanayohitajika bila kupoteza shangwe yetu.

Kwa hiyo, basi, kuwa na mengi ya kufanya hakumaanishi kwamba hatuwezi kuwa na furaha. Watu wenye shughuli nyingi zaidi wanaweza kuwa miongoni mwa watu wenye furaha zaidi ikiwa wao ni wenye kiasi, wenye kudumisha mtazamo mzuri, na wenye kutumia uamuzi mzuri ili kuendelea kuwa wenye usawaziko mzuri. Tunaweza kuona furaha nyingi zaidi iwezekanavyo ikiwa tunaonyesha hekima, tunafanya kazi nzuri, na kutegemeza tumaini letu juu ya Yehova Mungu.—1 Timotheo 6:17-19.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki