Sema Kweli na Jirani Yako
1 Mojawapo amri mbili kubwa zaidi ni: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.” (Mt. 22:39) Upendo huo utatusukuma tushiriki na jirani zetu kitu kizuri tulicho nacho—kweli ambayo tumepata katika Neno la Mungu. Kwa kuwa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hukazia ujumbe wa kweli wa Biblia, kupata maandikisho mwezi wa Mei ni njia moja ya ‘kusema kweli na jirani zetu.’—Efe. 4:25.
2 “Amkeni!” la Aprili 22 lapaswa kutolewa hadi ugavi wako wishe. Unaweza kuanza utoaji wako kwa kuuliza:
◼ “Itikio lako kwa ulimwengu usio na vita ni nini? [Ruhusu itikio.] Je, ulijua kwamba dini za ulimwengu huchochea vita na uuaji? [Ruhusu itikio.] Kwa kinyume kabisa, ona yale ambayo Biblia husema waabudu wa kweli wa Mungu watafanya.” Soma Isaya 2:2-4 kuanzia kwenye sehemu ya juu ya ukurasa 4 wa gazeti hilo, kisha kwenye ukurasa 10 usome fungu la kwanza chini ya kichwa kidogo “Kuwaita Wapendao Amani.” Kisha, uliza: “Je, wajua jinsi Mungu atakavyofanya hivyo? Jibu lapatikana katika gazeti hili, ambalo unaweza kuandikisha.”
3 Unapotoa “Mnara wa Mlinzi” la Mei 15, jaribu kuzungumzia tukio la habari ya karibuni ambalo limefanya watu wasihisi salama, kisha uulize:
◼ “Unafikiri ni nini kitakachohitajiwa ili kutufanya tuhisi salama katika maisha haya? [Ruhusu itikio.] Kusema wazi, je, ni jambo la akili kutumaini binadamu watatue matatizo yanayokabili wanadamu? [Ruhusu itikio; kisha usome Zaburi 146:3.] Mtunga-zaburi atoa sababu ya kuwa wenye kutazamia mazuri kuhusu wakati ujao. [Soma Zaburi 146:5, 6.] Makala hii, ‘Usalama wa Kweli, Sasa na Milele,’ yaeleza kwa nini twaweza kumtumaini Yehova Mungu alete hali bora duniani.” Toa andikisho na urudi kuzungumza jinsi inavyowezekana kufurahia maisha yenye usalama sasa.
4 Simulizi la jalada la “Amkeni!” la Mei 22 lapaswa kupendeza watu katika eneo la nyumba kwa nyumba na la kibiashara. Unaweza kulitoa kwa kusema:
◼ “Wanawake wengi wamepata tatizo la kusumbuliwa kingono kazini. Hali hiyo imekuwa mbaya sana hivi kwamba mahakama zimeanza kuadhibu wakosaji na kuamuru wadhulumiwa walipwe ridhaa. Tukitoa utumishi kwa jamii, tumechapisha ripoti hii, inayoondoa ngano zozote za kawaida kuhusu jambo hili. Pia yaandaa mawazo yatumikayo kwa wanawake na wanaume kuhusu jinsi ya kujilinda wasije wakawa wadhulumiwa au washtakiwa wa kusumbua kingono. Je, ungependa kusoma toleo hili la gazeti la Amkeni!?” Ruhusu itikio. Eleza kuhusu toleo la andikisho.
5 Ikiwa wapendelea utoaji mfupi, unaweza kujaribu huu:
◼ “Wengi huhisi kwamba magazeti yaliyo mengi yapendwayo leo hukazia sana biashara, ngono, au jeuri. [Onyesha Mnara wa Mlinzi na Amkeni!] Tunagawanya majarida haya yenye kujenga yategemeayo Biblia. Ni yenye kuelimisha sana na hutufundisha kumwabudu Mungu, kupenda jirani yetu, na kudumisha mwenendo mnyoofu. Ikiwa unapendelea habari ya kusoma ya aina hii, nina uhakika utafurahia yale utakayopata katika matoleo haya.”
6 Tukiwa wenye bidii katika kusema kweli na jirani zetu, huenda tukaweza kuletea wengi shangwe nyingi.—Mdo. 8:4, 8.