Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/98 uku. 1
  • Yehova Hupa Nguvu Ipitayo Iliyo ya Kawaida

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Hupa Nguvu Ipitayo Iliyo ya Kawaida
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • “Tafuteni Bwana na Nguvu Yake”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Yehova Humpa Nguvu Aliyechoka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Kazi Inayotegemezwa na Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • “Mwenyezi-Mungu . . . Amejaa Nguvu”
    Mkaribie Yehova
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 1/98 uku. 1

Yehova Hupa Nguvu Ipitayo Iliyo ya Kawaida

1 Wanafunzi wote wa Yesu wamekabidhiwa pendeleo lenye thamani la utumishi mtakatifu, yaani, huduma ya Kikristo. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Lakini kutokamilika kwa binadamu na msongo wa mfumo huu wa mambo nyakati nyingine huenda ukatusababisha tujione wenyewe kuwa tusiostahili kabisa.

2 Jambo hili litukiapo twaweza kufarijiwa na barua ya mtume Paulo aliyowaandikia Wakristo watiwa-mafuta katika Korintho. Aliandika hivi: “Tuna hazina hii katika vyombo vya udongo.” (2 Kor. 4:7) Paulo alikuwa na uhakika huu: “Kwa kuwa sisi tuna huduma hii . . . , hatufi moyo.” (2 Kor. 4:1) Wawe ni watiwa-mafuta au wa “kondoo wengine,” kwa kweli ni kichocheo kwa kila mmoja wetu cha kufuliza kutangaza habari njema na ‘si kufa moyo.’ Twahitaji nguvu kutoka kwa Mungu, ambaye hugawa “nguvu ipitayo iliyo ya kawaida.”—Yn. 10:16; 2 Kor. 4:7b.

3 Kwa kutia moyo, Mashahidi wengi ni waeneza-evanjeli wenye bidii ijapokuwa wanashindana na upinzani mkali, matatizo makubwa ya afya, au fedha chache. Sisi sote lazima tung’amue kwamba mgawo wetu wa kuhubiri unategemezwa na Yehova. Badala ya kuacha kivunjamoyo au wasiwasi udhoofishe azimio letu la kuhubiri, acheni “[twendelee] kujipatia nguvu katika Bwana na katika uwezaji wa nguvu yake.”—Efe. 6:10; Mit. 24:10.

4 Jinsi ya Kujipatia Nguvu ya Mungu: Dumu katika sala, ukiomba msaada na nguvu ya Mungu. (Rom. 12:12; Flp. 4:6, 7) Kisha, kwa moyo wako wote, mwitibari Yehova aandae nguvu ipitayo iliyo ya kawaida. (Mit. 3:5) Soma masimulizi ya maisha ya siku ya kisasa katika magazeti yetu, kwa kuwa hayo hutoa uthibitisho kwamba Yehova anasaidia watumishi wake leo wavumilie majaribu. Shirikiana kwa ukaribu na akina ndugu kutanikoni, na usiache mikutano ya kutaniko.—Rom. 1:11, 12; Ebr. 10:24, 25.

5 Na tufanye yote tuwezayo tujiweke katika hali ya kupokea nguvu ya Yehova—nguvu ipitayo iliyo ya kawaida na itakayotusaidia tusife moyo katika kazi yenye umaana zaidi ya kuhubiri Ufalme.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki