Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/04 uku. 1
  • Kazi Inayotegemezwa na Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kazi Inayotegemezwa na Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Hupa Nguvu Ipitayo Iliyo ya Kawaida
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Thamini Pendeleo Lako la Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Thamani Bora Zaidi ya Elimu ya Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Namna ya Kuwa Wahudumu Wenye Matokeo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 2/04 uku. 1

Kazi Inayotegemezwa na Mungu

1 Kati ya watumishi wa Mungu leo, ni wachache walio na elimu ya pekee, mali, na umaarufu katika mfumo wa sasa wa mambo. Kwa sababu hiyo, watu fulani huidharau huduma yetu. (Isa. 53:3) Hata hivyo, kazi ya elimu ya Biblia tunayofanya imewaletea mamilioni ya watu ulimwenguni pote faraja na tumaini. Watu wa kawaida wamewezaje kupata matokeo hayo makubwa? Ni kwa kutegemezwa na Mungu. (Mt. 28:19, 20; Mdo. 1:8) “Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu,” akaeleza mtume Paulo, “ili aviaibishe vitu vyenye nguvu.”—1 Kor. 1:26-29.

2 Wengi kati ya mitume na Wakristo wengine wa karne ya kwanza walikuwa “watu wasio na elimu na wa kawaida tu.” (Mdo. 4:13) Hata hivyo, walitimiza kwa ujasiri utume wao wa kuhubiri habari njema, na Yehova alibariki jitihada zao. Licha ya vizuizi na upinzani, ‘neno la Yehova lilizidi kukua na kusitawi katika njia yenye nguvu.’ Kazi hiyo haingeweza kuzuiwa kwa sababu ilitegemezwa na Mungu. (Mdo. 5:38, 39; 19:20) Mambo yamekuwa vivyo hivyo siku zetu. Hata upinzani mkali kutoka kwa watawala wenye nguvu haujaweza kuzuia habari njema zisiendelee kusitawi na kukua.—Isa. 54:17.

3 Mungu Ndiye Anayestahili Sifa: Je, tujivune kwa sababu ya pendeleo letu la kuwa wahudumu wa Mungu? Sivyo hata kidogo. Akirejelea huduma ya Kikristo, Paulo alisema: “Tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili nguvu zinazopita zile za kawaida ziwe za Mungu na si zile za kutoka ndani yetu wenyewe.” (2 Kor. 4:7) Paulo alitambua kwamba angeweza kutimiza huduma yake kwa kuwa alikuwa na nguvu kutoka kwa Mungu.—Efe. 6:19, 20; Flp. 4:13.

4 Sisi pia hutambua kwamba tunatimiza kazi ya kuhubiri kwa sababu tu ‘tumeupata msaada kutoka kwa Mungu.’ (Mdo. 26:22) Kupitia tangazo hilo la ulimwenguni pote, Yehova anatutumia kwa njia ya pekee kuyatikisa mataifa—ishara ya hukumu itakayotekelezwa karibuni. (Hag. 2:7) Tuna pendeleo kubwa kuwa “wafanyakazi wenzi wa Mungu” katika kazi kuu ya mavuno ya kiroho!—1 Kor. 3:6-9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki