Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Des. 15
“Wakati huu wa mwaka, watu wengi hufikiria kuhusu kuzaliwa kwa Yesu. Je, umewahi kujiuliza alikulia katika familia ya aina gani? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Luka 2:51, 52.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia mambo tunayoweza kujifunza kutokana na masimulizi ya Biblia kuhusu malezi ya Yesu.”
Amkeni! Des. 22
“Sote tunatamani kuona watoto wetu wakiishi maisha yenye furaha na mafanikio. Unafikiri watoto wanahitaji nini ili kukabiliana na ulimwengu huu wa leo wenye mikazo? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Methali 22:6.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia kile ambacho watoto wanahitaji na jinsi wazazi wanavyoweza kutimiza mahitaji hayo.”
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Watu wengi hutamani amani duniani. Je, unafikiri kwamba tutapata kuona mambo hayo yakitimizwa? [Soma Zaburi 46:9. Kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi jambo hilo litakavyotimizwa na kwa nini tunaweza kuwa na uhakika katika ahadi ya Mungu kuhusu ulimwengu usio na vita.”
Amkeni! Jan. 8
“Ulimwenguni pote, mamilioni ya watu wanaugua ugonjwa wa kihisia, kama vile kushuka moyo na hisia zinazobadilika-badilika. Muumba wetu anawajali sana watu hao. [Soma Zaburi 34:18.] Gazeti hili linazungumzia jinsi watu wanaougua wanavyoweza kusaidiwa. Pia linataja ahadi ya Biblia kwamba hivi karibuni ugonjwa utaondolewa.”