Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Des. 15
“Katika kipindi hiki, watu ulimwenguni pote husherehekea kuzaliwa kwa Yesu kwa njia mbalimbali. Je, unajua kwamba unabii wa Biblia unahusianisha kuzaliwa kwa Yesu na amani ya milele? [Ngojea jibu. Kisha usome Isaya 9:6, 7.] Gazeti hili linaeleza jinsi amani hiyo itakavyopatikana.
Amkeni! Des. 22
“Je, umetambua kwamba watu hukazia sana urembo? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linazungumzia hatari fulani zinazotokana na kuhangaikia sana urembo. Pia linakazia thamani ya urembo ulio bora.” Soma 1 Petro 3:3, 4.
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Dini nyingi hufundisha kwamba ni lazima watu wapende jirani zao. [Soma Mathayo 22:39.] Unafikiri, basi, ni kwa nini vita vingi na mapigano mengi yanahusisha dini? [Ngojea jibu.] Makala hii ya Mnara wa Mlinzi inazungumzia swali hili, Je, dini inaweza kuwaunganisha wanadamu?”
Amkeni! Jan. 8
“Ungejibuje swali hili? [Soma swali kwenye jalada, kisha ungojee jibu.] Mali za asili za dunia zinapungua haraka sana. Hata hivyo, ona ahadi hii yenye kutia moyo. [Soma Zaburi 104:5.] Makala hii ya Amkeni! inazungumzia jinsi sayari yetu itakavyorudishwa katika hali nzuri hivi karibuni.”