Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Des. 15
“Watu wengi hufikiria kuzaliwa kwa Yesu. Je, wajua kwamba kuna mambo muhimu zaidi tunayoweza kujifunza kutokana na simulizi la Biblia kuhusu kuzaliwa kwake? [Ngoja ajibu. Kisha fungua ukurasa wa 5, na usome 2 Timotheo 3:16.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi lachunguza baadhi ya mambo hayo.”
Amkeni! Dec. 22
“Je, wahisi kwamba wazazi wana sababu nzuri ya kuhangaikia watoto wao kwa sababu ya vitumbuizo vya leo vyenye jeuri? [Ngoja ajibu.] Wazazi wengi hutumia mstari huu wa Biblia uwe mwongozo wao. [Soma Zaburi 11:5.] Toleo hili la Amkeni! husaidia familia zichunguze hatari zinazohusiana na michezo ya kompyuta.”
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Watu wengi wanapofiwa na wapendwa wao au kuwa wagonjwa, mara nyingi wao hujiuliza, ‘Kwa nini Mungu ameruhusu jambo hili?’ Labda umewahi kujiuliza swali hilo. Biblia yaonyesha kwamba Mungu huwahurumia wale wanaoteseka. [Soma Isaya 63:9a.] Gazeti hili laeleza kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atakomesha mateso.”
Amkeni! Jan. 8
“Je, wafikiri serikali yapasa kuingilia uhuru wa kusema? [Ngoja jibu.] Vipi ikiwa uhuru huo wa kusema unahusisha kuongea na wengine juu ya dini, kama tunavyosoma hapa? [Soma Matendo 28:30, 31.] Hivi majuzi, swali hilo lilizushwa mbele ya Mahakama Kuu ya Marekani. Unaweza kusoma habari hiyo katika toleo hili la Amkeni!”