Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Des. 15
“Wakati huu wa mwaka, watu wengi hufikiria maneno ambayo malaika walitangaza Yesu alipozaliwa. [Soma Luka 2:14.] Je, unafikiri kwamba kutawahi kuwa na amani duniani? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi ambavyo Yesu ataleta amani ya kweli duniani hivi karibuni.”
Amkeni! Des.
“Maoni ya kidini kuhusu matumizi ya kileo hutofautiana sana. Unafikiri Mungu ana maoni gani kuhusu kutumia kileo? [Mruhusu ajibu.] Ingawa muujiza wa kwanza wa Yesu ulikuwa kugeuza maji yawe divai, Biblia inatoa onyo hili. [Soma Methali 20:1.] Makala hii inaeleza maoni yaliyosawazika kuhusu jambo hilo.” Mwonyeshe makala inayoanza kwenye ukurasa wa 18.
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Je, unafikiri mafanikio ya mtu yanapaswa kupimwa kwa kutegemea utajiri alio nao? [Mruhusu ajibu. Kisha soma 1 Timotheo 6:9, 10.] Ingawa Biblia haishutumu kuwa na pesa, inaonyesha kwamba mafanikio ya kweli hayategemei kuwa na utajiri. Gazeti hili linaeleza jambo hilo.”
Amkeni Jan.
“Je, unafikiri kwamba tutawahi kuona jambo hili likitendeka? [Soma Isaya 33:24. Kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza mambo ambayo yametimizwa na sayansi ya kitiba na jinsi ahadi ya Biblia itakavyotimizwa.”