Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Des. 15
“Wakati huu wa sikukuu, watu wengi hujaribu kuonyesha upole na huruma. Je, unafikiri dunia ingekuwa bora zaidi ikiwa watu wangeonyesha huruma kila siku? [Mruhusu ajibu. Kisha usome 1 Petro 3:8.] Gazeti hili linaeleza umuhimu wa huruma na linataja jinsi tunavyoweza kuonyesha huruma.”
Amkeni! Des.
“Je, unafikiri wapendwa wetu waliokufa wataishi tena? [Mruhusu ajibu.] Biblia inasema kwamba kuna tumaini baada ya kifo. [Soma Zaburi 68:20.] Gazeti hili linaonyesha ni kwa nini hatupaswi kuogopa kwamba kifo ndio mwisho kabisa wa uhai.”
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Watu wengi wanaomba Ufalme wa Mungu uje. Kwa mfano, ona sala hii inayojulikana ambayo Yesu aliwafundisha wanafunzi wake. [Soma Mathayo 6:9, 10.] Je, umewahi kujiuliza Ufalme huo ni nini na utakuja lini? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha maoni ya Biblia kuhusu jambo hilo.”
Amkeni! Jan.
“Sikuzote wanawake wamebaguliwa na kutendewa jeuri. Unafikiri ni kwa nini? [Mruhusu ajibu.] Hebu ona jinsi Biblia inavyowashauri waume wawatendee wake zao. [Soma 1 Petro 3:7.] Gazeti hili linaonyesha kupitia Biblia jinsi Mungu na Kristo wanavyowaona wanawake.”