Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jan. 15
“Watu wengi wanashangaa kuona kwamba sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya zimekuwa za kibiashara. Je, unafikiri watu wameacha kuzingatia mambo yanayofaa? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi ambavyo desturi za sikukuu zimebadilika-badilika kwa muda mrefu. Pia linaonyesha jinsi tunavyoweza kumheshimu Mungu na Kristo ifaavyo.” Soma Yohana 17:3.
Amkeni! Des. 22
“Miaka 85 iliyopita, idadi ya watu waliokufa kutokana na ugonjwa fulani wa kuambukiza katika majuma 24 inazidi idadi ya watu ambao wamekufa kutokana na ugonjwa wa UKIMWI katika miaka 24. Watu fulani wamesema kwamba ugonjwa huo ndio tauni mbaya zaidi katika historia. Je, umewahi kusikia kuhusu homa ya Hispania? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia uwezekano wa kutokea tena kwa ugonjwa kama huo. Pia linatupa sababu ya kuwa na tumaini.” Soma Isaya 33:24.
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Wanadamu wanaweza kufanya mambo mengi mema, hata hivyo wamefanya maovu kupindukia. Umewahi kujiuliza kwa nini wanafanya maovu? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linatoa jibu la Biblia. Pia linaeleza jinsi wema utakavyoshinda uovu hatimaye.” Soma Waroma 16:20.
Amkeni! Jan.
“Umewahi kujiuliza hali ya ulimwengu itakuwaje miaka 20 au 30 ijayo? [Mruhusu ajibu, kisha usome Zaburi 119:105.] Biblia inafunua matukio ya wakati ujao na kutuwezesha kufahamu yale yatakayotukia. Gazeti hili linazungumzia unabii mbalimbali unaoonyesha umuhimu wa wakati tunamoishi na pia sababu za kutarajia mema.”