Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/98 uku. 1
  • Ziara Iwezayo Kuwa Baraka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ziara Iwezayo Kuwa Baraka
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • “Lichungeni Kundi la Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Wazee Hulitumikia Kutaniko Jinsi Gani?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Jinsi Ambavyo Wachungaji Wakristo Hukutumikia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Lichungeni Kundi la Mungu Lililo Chini ya Uangalizi Wenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 7/98 uku. 1

Ziara Iwezayo Kuwa Baraka

1 Zakayo alimpokea Yesu kwa shangwe awe mgeni nyumbani kwake. Nayo ziara hiyo ilipata kuwa baraka kama nini!—Luka 19:2-9.

2 Leo, akiwa Kichwa cha kutaniko, Yesu Kristo huelekeza wazee ‘wachunge kundi la Mungu.’ (1 Pet. 5:2, 3; Yn. 21:15-17) Zaidi ya kufundisha kwenye mikutano na kuongoza katika utumishi wa shambani, waangalizi wa kutaniko huandaa msaada wenye upendo, wa kibinafsi kwa washiriki mmoja-mmoja wa kutaniko. Kwa hiyo, mara kwa mara, huenda ukatazamia kupokea uangalifu wa kibinafsi kutoka kwa wazee, ama nyumbani mwako, ama kwenye Jumba la Ufalme, mnapokuwa pamoja katika utumishi wa shambani, au pindi nyinginezo. Je, wapaswa kuwa na wasiwasi kuhusu ziara za wazee? La, sivyo. Wanapokutembelea haimaanishi kwamba unapungukiwa katika njia fulani. Basi, kusudi la ziara ya uchungaji ni nini?

3 Paulo alisema alitaka kuwazuru akina ndugu ‘aone jinsi walivyo.’ (Mdo. 15:36) Naam, wakiwa wachungaji wenye upendo, wazee wanapendezwa sana na jinsi ulivyo. Wanataka kutoa msaada wa kiroho ambao huenda ukakusaidia na kukujenga. Utunzaji wa kibinafsi wa jinsi hiyo ndio ambao Mchungaji wetu mwenye upendo Yehova hutaka tuwe nao.—Eze. 34:11.

4 Karibisha Ziara za Wazee: Mradi wa Paulo wa kuwazuru ndugu zake ulikuwa ‘kuwapa baadhi ya zawadi ya kiroho kusudi wafanywe imara, kwamba kupate kuwa na badilishano la kitia-moyo.’ (Rom. 1:11, 12) Sisi sote twahitaji kitia-moyo cha kiroho katika siku hizi za mwisho zilizo ngumu, nasi twahitaji msaada ili tuendelee kuwa imara katika imani. Itikio lako lifaalo kwa ziara za wachungaji bila shaka litatokeza badilishano zuri la kitia-moyo.

5 Thamini manufaa nyingi zipatikanazo kutoka katika kazi ya uchungaji ya wazee. Ikiwa kuna jambo fulani au swali ambalo lakuhangaisha, kumbuka kwamba wazee wako kutanikoni ili kusaidia. Usisite-site kuzungumza nao mambo yoyote ambayo huenda yakawa yanaathiri hali yako njema ya kiroho. Thamini mpango huu wenye upendo uliofanywa na Yehova, upate shangwe ambayo ziara hiyo yaweza kuleta.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki