Jirani Zetu Wahitaji Kusikia Habari Njema
1 Ni mapenzi ya Mungu “kwamba watu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:4) “Watu wa namna zote” wangetia ndani jirani zetu wote. Kuwafikia na habari njema kwataka kubadili utoaji wetu na kuhangaikia yale ambayo huenda yakampendeza kila mtu tunayekutana naye. (1 Kor. 9:19-23) Tengenezo la Yehova limeandaa vyombo vinavyoweza kutusaidia tufikie mioyo ya wale ‘walio na mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele.’ (Mdo. 13:48) Acheni tuone jinsi tunavyoweza kutumia broshua mbalimbali Julai na Agosti kushughulikia mahitaji ya kiroho ya jirani zetu.
2 Broshua Zilizokaziwa: Hapa chini utapata madokezo yaliyoorodheshwa ambayo labda yatakusaidia utakapokuwa ukitoa broshua kadhaa. Kila dokezo latia ndani (1) Swali lenye kuvuta fikira la kuanzisha mazungumzo, (2) rejezo ambamo mambo ya kuzungumzia yanaweza kupatikana katika broshua, na (3) andiko lifaalo ambalo laweza kusomwa wakati wa mazungumzo. Waweza kujazia sehemu iliyobaki ya utoaji kwa maneno yako mwenyewe, kulingana na itikio la mtu. Kuhusu broshua zilizo nyingi, toleo la wakati uliopita la Huduma ya Ufalme Yetu latajwa ambapo utapata utoaji wenye mambo mengi wa broshua hiyo.
Je! Kweli Mungu Anatujali?
Unafikiri kuna tumaini gani la kusaidia watu ambao wametendwa vibaya?—Ukurasa wa 27-28, fungu la 23-27; Isa. 65:17, 18; km-SW 7/97 uku. 4.
Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?
Kwa nini leo watu wengi wanaonekana kuwa wasiotosheka na maisha zao?—Ukurasa wa 29-30, fungu la 2, 25-26; Zab. 145:16; km-SW 7/96 uku. 4.
Furahia Milele Maisha Duniani!
Je, umepata kujiuliza Yesu Kristo anafanya nini sasa?—Picha 41-42; Ufu. 11:15; km-SW 8/96 uku. 8.
Serikali Itakayoleta Paradiso.
Je, ungependa kujua habari ya Ufalme ambao Yesu alitufundisha kusali kuuhusu?—Ukurasa wa 3; Mt. 6:9, 10; km-SW 8/96 uku. 8.
Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa.
Je, umepata kujiuliza jinsi utakavyomfariji mtu fulani ambaye amepoteza mpendwa katika kifo?—Ukurasa wa 26, fungu la 2-5; Yn. 5:28, 29; km-SW 7/97 uku. 4.
Je! Uamini Utatu?
Je, kuamini kwetu hali ya kweli ya Mungu ni kwa maana kwa ajili ya wakati wetu ujao?—Ukurasa wa 3, fungu la 3, 7-8; Yn. 17:3.
3 Broshua Nyingine: Nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Februari 1998 yaorodhesha vichapo vingine, kutia ndani broshua, ambazo hasa zimekusudiwa kutumiwa kutolea ushahidi Wabudha, Wahindu, Wayahudi, na Waislamu. Mahali pafaapo, broshua hizo zaweza kutolewa kwa watu tunaokutana nao. Waweza kupitia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4-6 katika nyongeza hiyo pamoja na ukurasa wa 21-24 katika kitabu Kutoa Sababu na usitawishe utoaji mfupi unaoweza kuvutia kupendezwa kwa watu hao.
4 Broshua nyingine imetayarishwa ili kuwasaidia watu ambao huenda wakawa wameelimishwa vizuri lakini hawajui mengi kuhusu Biblia. Imekusudiwa kuwachochea watake kulichunguza Neno la Mungu. Inapofaa, waweza kuchagua kutoa ifuatayo:
Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote.
Je, utakubali kwamba kupata elimu pana hutia ndani kupata ujuzi fulani juu ya yaliyomo katika Biblia?—Ukurasa wa 3, fungu la 1-3 na ukurasa wa 30, fungu la 2; Mhu. 12:9, 10.
5 Broshua ya Funzo la Biblia: Lengo letu katika huduma sikuzote lapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia, ama kwenye ziara ya kwanza au kwenye ziara ya kurudia. Tukiwa na lengo hilo, tuna broshua ifuatayo iliyo rahisi kutumia kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia nyumbani:
Mungu Anataka Tufanye Nini?
Je, ulipata kujua kwamba kwa dakika 30 au zisizozidi hizo kila juma kwa majuma 16, unaweza kupata uelewevu wa msingi wa Biblia?—Somo la 2, fungu la 6; 2 Tim. 3:16, 17; km-SW 3/97 uku. 4.
6 Katika kielezi cha Yesu cha Msamaria mwenye ujirani, Yesu alionyesha wazi kwamba jirani wa kweli ni yule adhihirishaye upendo na fadhili kumsaidia mwingine katika taabu. (Luka 10:27-37) Jirani zetu wamo katika taabu ya kiroho. Wanahitaji kusikia habari njema. Na tuchukue daraka la kuzishiriki pamoja nao, hivyo tukijithibitisha wenyewe kuwa wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo.—Mt. 24:14; Gal. 5:14.