Tumia Broshua Uvutie Akili na Moyo
1 Kweli ya Biblia yapaswa kutolewa ili kuvutia akili na moyo. Yesu alipofafanua kweli kwa wasikilizaji wake, alichagua habari zilizowapendeza na kuwachochea. (Luka 24:17, 27, 32, 45) Kufanikiwa kwa huduma yetu kwategemea sana jitihada tunayoweka kutambulisha mahitaji ya kiroho ya wasikilizaji wetu.
2 Broshua zaweza kuwa zenye matokeo kwa kuvutia akili na moyo wa wale tunaokuta katika huduma. Fikiria kimbele mtu ambaye huenda akakubali ujumbe ulio katika kila broshua inayotolewa katika Agosti:
—Je! Mungu Anatujali? Watu ambao wamepatwa na mshuko wa kiuchumi au ambao wamepatwa na msiba watathamini ujumbe huu wenye kufariji kuhusu wakati ujao usio na mateso.
—Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje? Vijana wanaofikiria kwa uzito wakati wao ujao watanufaika na majibu yanayotegemea Biblia yanayopatikana katika broshua hii.
—Furahia Milele Maisha Duniani! Picha nyingi na maandiko yaliyoonyeshwa yatasaidia watoto wachanga na wale walio na uwezo mdogo wa kusoma, kuelewa makusudi ya Mungu.
—Serikali Itakayoleta Paradiso. Mtu yeyote anayehusika na serikali huenda akakubali ujumbe huu kuhusu jinsi Ufalme wa Mungu utakavyotatua matatizo magumu ya wanadamu.
—Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Waelekezaji wengi wa maziko huthamini kuwa na nakala za broshua hii kwa ajili ya familia zilizofiwa. Wahubiri wanaotoa ushahidi makaburini hutumia broshua hii kufariji waombolezaji. Dada wawili waliifikia familia ya watu saba ambao walikuwa wakisali kando ya kaburi. Tokeo la kushiriki ujumbe huo wenye kufariji kutoka katika broshua hiyo ni kwamba, funzo la Biblia lilianzishwa na mama siku iliyofuata!
—Je! Uamini Utatu? Huenda mtu wa kidini akakubali kweli inayopatikana katika ufichuaji huu wenye uthibitisho wa kutosha wa fundisho kuu la Jumuiya ya Wakristo.
3 Ifahamu kila broshua, na uamue jinsi unavyoweza kuitumia ifaavyo zaidi katika eneo lako. Ili kupata utoaji mbalimbali uliodokezwa, ona ukurasa wa nyuma wa toleo la Julai 1998 la Huduma ya Ufalme Yetu. Yehova na abariki jitihada zako za kufikia akili na mioyo ya watu.—Mr. 6:34.