Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/99 uku. 4
  • Toa Kitabu Furaha ya Familia kwa Watu wa Kila Umri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Toa Kitabu Furaha ya Familia kwa Watu wa Kila Umri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Kusaidia Familia Zipate Wakati Ujao Wenye Kudumu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kushiriki na Wengine Siri ya Kupata Furaha ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Madokezo ya Utoaji wa Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Ujuzi Kutoka kwa Mungu Hujibu Maswali Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 2/99 uku. 4

Toa Kitabu Furaha ya Familia kwa Watu wa Kila Umri

1 Mvulana mwenye umri wa miaka 11 kutoka California alieleza uthamini wake kwa kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Yeye aliandika hivi: “Nashukuru sana kwa ajili yake, natia moyo familia nyingine zisome kitabu hiki kwa sababu ni kizuri sana. Pia . . . kinasaidia familia yetu ipate amani na furaha nyumbani kwetu.” Jambo lililoonwa la kijana huyo lapaswa kututia moyo tutoe kitabu Furaha ya Familia kwa watu wa kila umri. Haya ni madokezo machache ambayo huenda ukataka kujaribu katika huduma yako Februari.

2 Unapompata kijana, waweza kusema:

◼ “Wengi wa rika lako wanafikiria kufunga ndoa. Lakini waweza kupata wapi habari yenye kutegemeka juu ya ndoa? [Ruhusu jibu.] Mara nyingi vijana husema kwamba hawana uhakika kama wako tayari kufunga ndoa. Acha nishiriki nawe yale ambayo kitabu hiki husema juu ya habari hii.” Fungua ukurasa wa 14 katika kitabu Furaha ya Familia, na usome fungu la 3. Kisha eleza kila kichwa kidogo katika sura hiyo. Toa kitabu kwa mchango wa kawaida, na upange kurudi.

3 Unapozungumza na mzazi, waweza kusema:

◼ “Tunashiriki na wazazi miongozo fulani inayotumika kikweli katika kulea watoto. Hiyo imekusanywa katika kitabu hiki kidogo Siri ya Kupata Furaha ya Familia.” Fungua ukurasa wa 55. Soma fungu la 10, pia Kumbukumbu la Torati 6:6, 7, katika fungu la 11. Kisha kazia sentensi zilizopigwa chapa za mlazo katika fungu la 12 hadi 16. Endelea, kwa kusema hivi: “Kitabu hiki kimesaidia watu wengi wafanikiwe zaidi wakiwa wazazi. Ikiwa ungependa kukisoma, nitafurahi kukupatia nakala hii kwa mchango wa——.”

4 Unapozungumza na mzee-mzee, waweza kusema:

◼ “Baada ya kusoma maelezo haya mafupi, tafadhali niambie unavyofikiri.” Fungua kitabu Furaha ya Familia kwenye ukurasa wa 169, na usome sentensi mbili za kwanza za fungu la 17. Kisha mwombe atoe maelezo. Ikitegemea jibu, waweza kusoma madondoo zaidi kutoka katika kitabu hicho kabla ya kukitoa.

5 Unapofuatia maangusho ya kitabu Furaha ya Familia, kumbuka kuanzisha funzo la Biblia. Somo la 8 katika broshua Anataka au sura ya 5 katika kitabu Ujuzi huenda zikafaa kuanza nazo. Wakati huohuo, na tujitahidi kusaidia watu wa kila umri kujenga maisha ya familia ya Kikristo yenye furaha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki