Kusaidia Familia Zipate Wakati Ujao Wenye Kudumu
1 “Pupa inafaa,” mwanauchumi mmoja akaliambia darasa la chuo lenye kuhitimu, akiongezea: “Unaweza kuwa mwenye pupa na bado ujihisi vizuri.” Hivyo ndivyo ulimwengu huendeleza kujipendeza kuwa njia ya kujihakikishia wakati ujao. Kwa tofauti iliyo wazi, Yesu alifundisha kwamba Mkristo lazima “ajikane mwenyewe . . . kwa maana itakuwa manufaa gani kwa mtu ikiwa atapata faida ya kuwa na ulimwengu wote lakini aipoteze nafsi yake?” (Mt. 16:24-26) Ili kujipatia wakati ujao ulio salama, lazima mtu akazie maisha yake kufanya mapenzi ya Mungu—mradi wa maana zaidi kwa familia leo. (Zab. 143:10; 1 Tim. 4:8) Ujumbe huo wawasilishwa kwenye sura ya kumalizia ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Kichapo hiki kipya chasaidia watu kuona jambo lililo la maana maishani na jinsi wanavyoweza kutenda kwa manufaa kuelekea familia zao. Tunapoendelea kuhubiri habari njema kila mahali, twaweza kusema nini ambacho kitatia moyo wale tunaokuta wasome kitabu Furaha ya Familia? Haya ni madokezo kadhaa:
2 Mlangoni na hata barabarani, unaweza kujaribu kutumia trakti “Furahia Maisha ya Familia” kuanzisha mazungumzo. Unaweza kuuliza:
◼ “Kukiwa na mahangaiko yote ambayo maisha ya kisasa hutuletea, je, wafikiri inawezekana kuwa na maisha ya familia yenye furaha kweli? [Ruhusu itikio.] Trakti hii hutuhakikishia kwamba inawezekana. Je, ungependa kuisoma?” Ikikubaliwa, unaweza kuendelea kusema: “Kwa kuwa unapendezwa na jambo hili, labda pia utafurahia kitabu hiki ambacho huandaa ushauri wenye kina wa jinsi ya kupata furaha katika familia.” Onyesha yaliyomo katika kitabu Furaha ya Familia. Onyesha vichwa vya sura vichache vyenye kuvutia. Fungua ukurasa wa 10, na usome kuanzia sentensi ya mwisho ya fungu la 17 hadi mwisho wa fungu la 18. Toa kitabu. Eleza kwamba una mengi ya kushiriki, na uulize ni lini unapoweza kurudi tena.
3 Unaweza kufuatia mazungumzo yako ya kwanza kuhusu maisha yenye furaha ya familia kwa kusema:
◼ “Ningependa kukuonyesha jambo fulani katika kitabu ulichopata ambalo nafikiri utalithamini. Sura ya mwisho yakazia siri yenyewe ya furaha ya familia. [Soma fungu la 2 kwenye ukurasa wa 183.] Angalia kwamba kujitahidi pamoja kufanya mapenzi ya Mungu ndio ufunguo. Twapendekeza kwamba familia zijifunze Biblia pamoja zijue mapenzi ya Mungu ni nini na jinsi ya kuyatumia katika nyumba yao. Twatoa mtaala wa funzo la Biblia bila malipo ambao huchukua miezi michache tu kuumaliza. Ukiniruhusu, nitakuonyesha jinsi linavyoongozwa.” Rudi ukiwa na broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? au kitabu Ujuzi, chochote kitakachofaa zaidi.
4 Unapoongea na wanadarasa wenzako shuleni au vijana katika eneo, huenda ukapata itikio kwa swali hili:
◼ “Ni jambo la maana kadiri gani kwa wazazi na watoto wao kudumisha mawasiliano? [Ruhusu itikio.] Ona jinsi kitabu hiki kuhusu maisha ya familia kinavyosema juu ya somo la ‘Uwasiliano wa Haki na Ulio Wazi.’ [Soma fungu la 4 lote, ukikazia andiko la Mithali 15:22, na sentensi ya kwanza ya fungu la 5 kwenye ukurasa wa 65 katika kitabu Furaha ya Familia.] Mafungu yanayofuata yanaandaa madokezo yenye kutumika ya jinsi ya kuboresha mawasiliano katika familia. Kitabu hiki kina kichwa Siri ya Kupata Furaha ya Familia.” Eleza kwamba utarudi baadaye ujue maelezo yake juu ya yale anayosoma.
5 Unaweza kujenga mazungumzo yako ya kwanza pamoja na kijana kuhusu mawasiliano kati ya mzazi na mtoto kwa kusema:
◼ “Nilithamini kupendezwa ulikoonyesha katika umaana wa kuwa na mawasiliano mazuri katika familia yenu. Je, ungesema ni nini iliyo habari ya maana zaidi ambayo wazazi na watoto wanapaswa kuzungumza?” Ruhusu itikio. Kisha fungua ukurasa wa 68 katika kitabu Furaha ya Familia, na usome jibu linalopatikana katika nusu ya kwanza ya fungu la 11. “Kuwa na funzo la Biblia la kila juma ni njia bora kabisa ya kujipatia ujuzi juu ya Mungu.” Toa broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Eleza kwamba masomo yayo 16 huandaa muhtasari wa msingi wa ujumbe wa Biblia. Soma utangulizi kwenye ukurasa wa 2, kisha zungumzeni pamoja somo la kwanza.
6 Ukimkuta mzazi katika mahubiri ya nyumba hadi nyumba, au labda kwenye bustani au mahali pa kuchezea, unaweza kuamsha kupendezwa kwa kusema:
◼ “Nina hakika utakubali kwamba kulea watoto leo ni jambo gumu sana. Unafikiri ni nini kiwezacho kulinda watoto wako na mavutano yasiyofaa? [Ruhusu itikio.] Hapa pana ushauri bora kabisa ambao nimethamini.” Simulia kielezi katika fungu la 1, na usome fungu la 2 kwenye ukurasa wa 90 katika kitabu Furaha ya Familia. Eleza jinsi kinavyotoa mwelekezo wenye matokeo kulinda familia na mavutano yenye kuharibu. Acha kitabu, na uwe tayari kujibu swali lolote linalotokea.
7 Katika ziara yako ya pili kwa mzazi aliyekubali kitabu “Furaha ya Familia,” unaweza kuendeleza mazungumzo kwa njia hii:
◼ “Tulipokutana mara ya kwanza, niliweza kuona kwamba unajali kikweli kuhusu watoto wako na kwamba unataka kufanya yote uwezayo kuwalinda na mavutano mabaya. Huenda bado hujasoma kile kitabu nilichokuachia, lakini kuna maoni ya maana ndani yacho unayopaswa kuona. [Soma fungu la 19 kwenye ukurasa wa 59.] Kusitawisha uhusiano pamoja na Mungu kwahitaji kumjua kupitia Neno lake lililoandikwa, Biblia. Je, ungependa nikuonyeshe jinsi tunavyojifunza Biblia tukiwa familia?”
8 Washauri wa kilimwengu hawawezi kuonyesha familia njia ya kupata furaha bali kwa hakika watawatamausha. Na tugawanye sana kitabu Furaha ya Familia hivi kwamba watu kila mahali waweza kusaidiwa na Neno la Mungu wapate wakati ujao wenye kudumu.—1 Tim. 6:19.