Je, Tutoe Kitabu Muumba?
Sisi sote tulifurahia kupokea kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Kitabu hicho kimekusudiwa hasa wale ambao, ijapokuwa wana elimu ya juu kuhusu mambo ya kilimwengu, huenda ikawa hawamwamini Mungu. Kitabu hiki chashughulika na uhitaji wenye kuongezeka daima.
Kwa sababu zenye kutumika, toleo la fasihi la kila mwezi sikuzote huwa vichapo vyenye kuvutia sana. Je, hiyo yamaanisha kwamba tuepuke kutoa kitabu Muumba? Sivyo hata kidogo! Kitabu hiki chaweza kutolewa wakati wowote mwakani kwa watu ambao hawamwamini Mungu na ambao huenda wakanufaika nacho. Pia huenda kikatolewa kwa watu wanaomwamini Mungu lakini wasiomjua kabisa au wasiojua sifa zake na makusudi yake. Kwa hiyo, unatiwa moyo kubeba nakala moja katika mkoba wako wa mahubiri na kuwa tayari kukitolea mtu yeyote unayefikiri atapendezwa kukisoma.