Biblia Inafundisha—Kitabu Chetu Kikuu cha Kufundishia Biblia
1 Tulisisimuka sana tulipopokea kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kwenye Kusanyiko la Wilaya la “Utii wa Kimungu.” Wahudhuriaji walifurahi kupokea kitabu hicho baada ya hotuba ya mwisho siku ya Jumamosi. Tutakitumiaje? Kitabu hicho ndicho tutakachotumia hasa kufundisha Biblia. Ijapokuwa tutakitoa shambani kwa mara ya kwanza mwezi wa Machi, wahubiri wanatiwa moyo waanze kukitumia mara moja ili kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia.
2 Mafunzo ya Biblia Ambayo Tayari Yameanzishwa: Wahubiri wanaoongoza mafunzo ya Biblia katika kitabu Ujuzi au broshua Anataka wanapaswa kutumia busara kuamua jinsi na wakati wa kuanza kutumia kitabu hicho kipya kuongoza mafunzo hayo. Ikiwa funzo lilianzishwa majuzi, unaweza kuanza na sura ya kwanza ya hicho kitabu kipya. Ikiwa funzo limeendelea kwa muda, mnaweza kuanza na sura ya kitabu Biblia Inafundisha inayolingana na sura ambayo mmefikia katika Ujuzi. Ikiwa mmefikia sura za mwishomwisho za kitabu Ujuzi, huenda ikafaa kumaliza kujifunza kitabu hicho.
3 Bila shaka sisi sote tunawajua watu wengi ambao wangenufaika kwa kujifunza kitabu Biblia Inafundisha. Basi mtolee kila mtu funzo la Biblia katika kitabu hicho kinachofafanua mafundisho ya Biblia hatua kwa hatua. Kwa mfano, wale ambao tayari wamejifunza broshua Anataka au kitabu Ujuzi lakini hawajajiweka wakfu na kubatizwa huenda wakataka kuendelea na funzo katika kitabu hicho kipya. Wazazi wanaweza kukitumia wanapowafundisha watoto wao ili wawe na ujuzi sahihi kuhusu mapenzi ya Mungu.—Kol. 1:9, 10.
4 Kujifunza Kitabu cha Pili: Je, mwanafunzi atajifunza kitabu cha pili baada ya kujifunza kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ndiyo. Mwanafunzi akifanya maendeleo, hata kama ni ya polepole, na anathamini yale anayojifunza, mnaweza kuendelea kujifunza kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli. Tuna hakika kwamba kitabu Biblia Inafundisha kitatusaidia sana tunapojitahidi kutii amri ya kufanya wanafunzi.—Mt. 28:19, 20.