Tumia Kitabu Mwabudu Mungu Kuongoza Mafunzo ya Biblia
Kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli kinakusudiwa kuwasaidia wapya wafanye maendeleo katika kweli na kumthamini zaidi Yehova na tengenezo lake. Kinaweza kutumiwa kama kitabu cha pili cha funzo. Ukurasa wa 4 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2000 ulieleza hivi: “Kama ni dhahiri kwamba mtu huyo anafanya maendeleo, ingawa polepole, na kwamba anathamini yale anayojifunza, basi endeleza funzo la Biblia kupitia kitabu cha pili baada ya kumaliza broshua Anataka na kitabu Ujuzi. . . . Wakati wote, broshua Anataka na kitabu Ujuzi ndivyo vitakavyotumiwa kujifunzia kwanza. Funzo la Biblia, ziara za kurudia, na wakati unaotumiwa kuendeleza funzo wapaswa kuhesabiwa na kuripotiwa, hata kama mwanafunzi amebatizwa kabla ya kumaliza kujifunza kitabu cha pili.”
Ni nani wengine wanaoweza kunufaika kwa kujifunza Biblia kupitia kitabu Mwabudu Mungu? Makala hiyohiyo yaendelea kusema: “Ikiwa unajua watu fulani ambao walijifunza [broshua Anataka na] kitabu Ujuzi zamani lakini hawajafikia kujiweka wakfu na kubatizwa, unaweza kuchukua hatua ya kuona kama wangependa kurudia funzo lao la Biblia.” Na tujitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia kupitia kitabu Mwabudu Mungu na watu hao mwezi wa Aprili.