Sanduku La Swali
◼ Ni vichapo gani tunavyopaswa kujifunza na wapya kabla ya ubatizo wao?
Kabla ya mtu kuweza kuweka maisha yake wakfu kwa Yehova na kubatizwa, lazima atwae ujuzi sahihi. (Yn. 17:3) Atapokea habari anayohitaji kwa kujifunza vichapo vyote viwili, broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? na pia kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Katika visa vingi broshua Anataka itasomwa kwanza. Hata hivyo, ikiwa funzo lilianzishwa katika kitabu Ujuzi, broshua Anataka yapasa kufuata katika funzo baada ya kitabu kukamilika. Kwa nini jambo hilo ni la lazima?
Broshua Anataka huandaa pitio la jumla la mafundisho ya msingi ya Biblia. Ikisomwa kwanza, itampa mwanafunzi uelewevu wa msingi wa matakwa ya kumpendeza Yehova. Ikisomwa mwisho, itakuwa pitio zuri la yale aliyojifunza katika kitabu Ujuzi. Kwa vyovyote vile, mtie moyo mwanafunzi achunguze na kutafakari maandiko yenye kuunga mkono somo. Hakikisha unakazia picha, kwa kuwa ni misaada yenye matokeo sana ya kufundisha.—Ona Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1997, ukurasa wa 16-17.
Mwanafunzi wa Biblia amalizapo kujifunza vichapo vyote viwili, huenda akaweza kujibu maswali yote ambayo wazee watapitia naye anapojitayarisha kwa ubatizo. Ikiwa hivyo, huenda lisiwe jambo la lazima kuongoza funzo rasmi naye katika kichapo kinginecho, ijapokuwa mwenye kuliongoza apaswa kuendelea kupendezwa kikweli na maendeleo yake.—Ona Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1996, ukurasa wa 14, 17.