Mikutano Ya Utumishi Kwa Julai
TAARIFA: Huduma ya Ufalme Yetu itaratibu Mkutano wa Utumishi kwa kila juma wakati wa miezi ya mkusanyiko. Makutaniko yanaweza kufanya marekebisho yahitajiwayo ili kuruhusu uhudhuriaji wa Mkusanyiko wa Wilaya wa “Neno la Mungu la Kiunabii” na kwa ajili ya pitio la dakika 30 la mambo makuu ya programu kwenye Mkutano wa Utumishi juma litakalofuata. Pitio la siku kwa siku la programu ya mkusanyiko wa wilaya lapasa kugawiwa mapema ndugu watatu wenye sifa za ustahili ambao wataweza kukazia mambo makuu yenye kutokeza. Pitio hili lililotayarishwa vizuri litasaidia kutaniko likumbuke mambo makuu ya kutumia kibinafsi na shambani. Maelezo yoyote kutoka kwa wasikilizaji na mambo yaliyoonwa yaliyosimuliwa yapaswa yawe mafupi na ya moja kwa moja.
Juma Linaloanza Julai 5
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Toa maelezo juu ya ripoti ya utumishi wa shambani ya Machi ya nchini na ya kutaniko la kwenu.
Dak. 15: “Sali Upate Msaada wa Yehova.” Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Eleza jinsi ambavyo sala za moyoni za aina mbalimbali hutimiza fungu la maana katika huduma yenye matokeo. Omba wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa kuonyesha jinsi ambavyo sala za wakati ufaao zimewasaidia katika huduma yao.—Ona Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 1996, ukurasa wa 32.
Dak. 20: Tumia Vizuri Broshua na Vichapo vya Toleo la Pekee Vilivyopo Kutanikoni. Hotuba na maonyesho. Eleza sababu zinazofanya broshua ziwe vyombo vyenye thamani katika huduma yetu. Zinashughulika na habari zenye kupendeza zaidi kwa matokeo, hueleza kichwa kimoja cha msingi kwa ufupi, na kueleza mafundisho ya Kimaandiko kwa usahili. Taja broshua zinazotolewa mwezi huu, na uonyeshe zile zilizo nyingi kwenu. Toa maonyesho mawili au matatu ya utoaji mbalimbali mfupi unaotegemea madokezo yanayopatikana chini ya kichwa “Presentations” katika Watch Tower Publications Index, au wonyesho wa mambo hususa kutoka katika vichapo vya toleo la pekee yanayoweza kutumiwa kuvitoa.
Wimbo 181 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 12
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: “Utayarishaji wa Kimbele Huleta Shangwe.” Hotuba na mahoji. Eleza kwa nini utayarishaji ni muhimu kwa utumishi wa shambani na jinsi hutuwezesha kuona shangwe kuu katika yale tufanyayo. (Ona kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 39, fungu la 1-3.) Hoji wahubiri wawili au watatu wenye uwezo ambao wanasema jinsi ambavyo wao hujitayarisha kabla ya kwenda kwenye utumishi wa shambani na jinsi ambavyo kufanya hivyo kumewasaidia. Simulia jambo lililoonwa kutoka katika Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 1993, ukurasa wa 30, kuonyesha matumizi yenye matokeo ya kitabu Kutoa Sababu katika kujitayarisha kwa ajili ya huduma.
Dak. 20: “Acheni ‘Tuseme Waziwazi!’” Wasikilizaji wakishiriki na maonyesho. Pitia kila dokezo la mambo ya kusema ili wenye nyumba wasikilize mlangoni. Panga wahubiri wenye uzoefu watoe utangulizi kadhaa mbalimbali wenye matokeo. Omba wasikilizaji watoe madokezo ya ziada na kusimulia mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo yanayoonyesha utoaji wenye matokeo zaidi kwenu.
Wimbo 183 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 19
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: Kufurahia kichapo 1999 Yearbook. Mazungumzo kati ya mume na mke. Mume aeleza kwamba kichapo Yearbook kilichapishwa awali kikiwa kitabu mwaka wa 1927 na kwamba kwa zaidi ya miaka 70, kimetia ndani ripoti ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova. Wanapitia mambo makuu ya “1998 Grand Totals,” kwenye ukurasa wa 31. Kisha wazungumzia “A Letter From the Governing Body,” kwenye ukurasa wa 3-5, na kutoa maelezo ya jinsi watakavyotii kitia-moyo kilichotolewa. Mahali ambapo hakuna kichapo 1999 Yearbook, tumia kile cha 1998. Mahali ambapo kichapo hicho hakichapishwi katika lugha ya hapo, tumia habari yenye ripoti katika Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1999, ukurasa wa 12-15.
Dak. 20: Je, Ni Lazima Nijiunge na Tengenezo? Mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 311-315. Mara nyingi sisi hukuta watu wenye kupokea ujumbe wa Ufalme lakini ambao huchukia “kujiunga” na tengenezo la kidini. Pitia ufafanuzi wa neno “tengenezo” na mambo saba yanayotambulisha tengenezo linaloonekana la Yehova. Eleza kwa nini tengenezo hilo ni tofauti na yale mengine na jinsi kushirikiana nalo huleta baraka za kweli.
Wimbo 189 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 26
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Julai. Sanduku la Swali.
Dak. 10: “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.” Hotuba. Tangaza tarehe ya kusanyiko la mzunguko litakalofuata, ikiwa yajulikana. Tia moyo wapya wafikirie juu ya kubatizwa. Wahimize wote wahudhurie kila kipindi. Wakati huohuo, wakumbushe wote wahakikishe wanahudhuria vipindi vyote vya mkusanyiko wa wilaya wa mwaka huu.
Dak. 20: Je, Twafanya Wanafunzi? Mwangalizi wa utumishi azungumza na mtumishi wa huduma mmoja au wawili mambo yapatikanayo katika Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1996, ukurasa wa 19-22. Kazia sababu za Kimaandiko zinazofanya tuhitaji kutafuta wenye kustahili katika eneo letu na kuwafanya wanafunzi. (Mt. 10:11) Hao ndio wapigao kite kwa sababu ya uovu na hali zenye ukosefu wa kumwogopa Mungu wanazoona kuwazunguka na wanaoelekea kumtafua Yehova kabla ya siku ya hasira yake kulipuka. (Eze. 9:4; Sef. 2:2, 3) Miongoni mwao ni ‘wale wenye mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele.’ (Mdo. 13:48) Utume wetu ni kufanya wanafunzi, tukiwafundisha watu mambo yote ambayo Yesu aliamuru. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Ingawa huenda tukachochea kupendezwa kwa wale tunaokuta katika mahubiri ya nyumba hadi nyumba, ushahidi wa vivi hivi, na ushahidi wa barabarani, twafanya wanafunzi kwa huduma ya kufuatia—kwenye ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia. Eleza madokezo yenye kutumika ya jinsi hilo liwezavyo kufanywa.
Wimbo 14 na sala kumalizia.