Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/99 uku. 4
  • Tumia Wakati Wako kwa Matokeo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumia Wakati Wako kwa Matokeo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Tumia Wakati Wako kwa Hekima Katika Huduma
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Uwe Mwenye Matokeo Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani Inayotimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 6/99 uku. 4

Tumia Wakati Wako kwa Matokeo

1 Kila mtu ana kiwango kilekile cha wakati kila juma. Sehemu tunayotumia kueneza habari njema hasa ni yenye thamani kwa sababu ni wakati unaotumiwa katika kazi ya kuokoa uhai. (Rom. 1:16) Twaonyesha uthamini kwa jambo hili kwa kujitayarisha vema kwa ajili ya utumishi uliopangwa, kwa kufika kwenye mikutano ya utumishi kwa wakati, na kuondoka bila kukawia kwenda kwenye eneo. Ni afadhali twendelee kuhubiri badala ya kungoja. Kwa kuwa Yehova ametufundisha kwamba “kwa kila jambo kuna majira yake,” twahitaji kutumia wakati tuliotenga kwa ajili ya huduma kwa matokeo kwelikweli.—Mhu. 3:1.

2 Tumia Wakati Wako kwa Hekima: Sisi hupata baraka nyingi tunaposhikilia imara ratiba inayoruhusu tushiriki kwa ukawaida katika huduma ya shambani. Kwa kawaida, matokeo mazuri tunayopata hudumani yapaswa kulingana na wakati tunaotumia katika utumishi. Tukirekebisha kidogo kawaida yetu, je, twaweza kutumia wakati mwingi zaidi katika utumishi wa shambani? Kwa mfano, baada ya utendaji wa magazeti Jumamosi, je, twaweza kuchukua wakati wa ziada kufanya ziara chache za kurudia? Ikiwa tumekuwa katika huduma ya shambani kwa muda fulani Jumapili, je, twaweza kutumia wakati fulani pia kufanya ziara za kurudia au kuongoza funzo la Biblia? Je, ingewezekana kuongezea utendaji wetu wa nyumba hadi nyumba na kutoa ushahidi barabarani? Katika njia hizi na nyinginezo, huenda tukaweza kuboresha utumishi wetu.

3 Tunapokuwa katika huduma, twaweza kupoteza wakati wenye thamani tusipokuwa waangalifu. Bila shaka, hali za hewa zinapokuwa mbaya zaidi, pumziko fupi litatuburudisha na kutusaidia twendelee. Hata hivyo, uwe mwenye usawaziko, kwa kuwa pumziko kama hilo huenda lisiwe la lazima sikuzote.

4 Katika miaka ya karibuni imekuwa vigumu sana kupata watu nyumbani. Ili kukabiliana na hali hiyo, wahubiri wengi huenda mlango hadi mlango saa tofauti za mchana. Kwa nini usijaribu kutoa ushahidi baadaye alasiri au mapema jioni-jioni ikiwezekana?

5 Ni vema tusipozungumziana huku tukitoa ushahidi wa barabarani. Badala yake, simameni mbali na mtu na mwenzake na kuwafikia watu ili mwanzishe mazungumzo nao. Kwa njia hiyo wakati utatumiwa kwa matokeo zaidi na utapata shangwe kubwa kutokana na kazi hiyo.

6 Tafuta Fursa za Kutoa Ushahidi: Wakati mwenye nyumba mmoja aliposema kwamba hakupendezwa, Shahidi mmoja alimwuliza kama kulikuwa na mtu mwingine ambaye angeweza kuongea naye. Hilo liliongoza kwenye mazungumzo na mwanamume wa nyumba hiyo, ambaye alikuwa mgonjwa kwa miaka mingi naye alikuwa amekaa kitandani kwa muda mrefu. Tumaini lililo katika Neno la Mungu lilifanya upya kupendezwa kwake na uhai. Upesi akatoka kitandani, akaanza kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme, na kushiriki tumaini lake jipya na wengine!

7 Dada mmoja tineja alitumia dokezo la kwenda katika utumishi wa shambani saa moja kabla ya Funzo la Kitabu la Kutaniko. Alipofika kwenye mlango wa kwanza, alimkuta msichana mwenye umri wa miaka 13 aliyesikiliza kwa makini na kuchukua fasihi. Siku iliyofuata shuleni, dada huyo mchanga alimwona msichana yuleyule. Upesi baada ya hapo, alijitolea kujifunza Biblia naye, na msichana huyo akakubali.

8 Ufanye Uwe Wakati Bora: Kushiriki kikawaida katika utumishi wa shambani hutusaidia kusitawisha stadi katika kutoa habari njema. Je, unaweza kuboresha uwezo wako wa kuanzisha mazungumzo mlangoni kwa kutumia utangulizi wenye matokeo zaidi? Je, waweza kuwa mwalimu mwenye ustadi unapoongoza funzo la Biblia nyumbani? Kwa kufanya hivyo, kwa kweli unaweza kutumia wakati wako katika utumishi kwa njia yenye matokeo na kufanya huduma yako iwe yenye matokeo zaidi.—1 Tim. 4:16.

9 Kwa kuwa “wakati ubakio umepunguzwa,” maisha yetu yapaswa kujaa kazi za Kikristo. (1 Kor. 7:29) Kutenga wakati wa kuhubiri kwapaswa kuwe jambo la kwanza katika orodha ya mambo yetu ya kutangulizwa. Na tushiriki ifaavyo, kwa bidii katika huduma. Wakati ni mali nzuri ajabu ambayo Yehova ametupa. Utumie kwa hekima sikuzote na kwa matokeo.

[Sanduku katika ukurasa wa 4]

Fikiria Madokezo Haya:

◼ Fika kwenye mikutano ya utumishi kwa wakati.

◼ Fanyeni vikundi vya kutoa ushahidi viwe vidogo, kwa kiasi.

◼ Epuka kuchelewa kufika kwenye eneo.

◼ Hubirini eneo wakati ambapo kuna watu wengi nyumbani.

◼ Hubiri peke yako wakati mwingine, ikiwa kuna usalama.

◼ Fanyeni ziara za kurudia karibu na eneo la kwenda mlango hadi mlango.

◼ Endelea na utumishi wengine katika kikundi wakawiapo mlangoni.

◼ Inapowezekana, ikitegemea hali, hubiri zaidi ya muda wa saa moja.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki