Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/99 uku. 3
  • Je, Waweza Kusaidia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Waweza Kusaidia?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Watie Moyo Wanawake Wakristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Je, Unawatendea Wanawake Kama Yehova Anavyowatendea?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Je! Wewe Waweza Kusaidia Wajane na Yatima “Katika Shida Zao”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Kutumia Neno la Mungu Katika Jamaa Zetu Wenyewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 6/99 uku. 3

Je, Waweza Kusaidia?

1 Mtume Paulo alionya kwa upole washiriki wa kutaniko ‘wawe na utunzaji uleule kwa mmoja na mwenzake.’ (1 Kor. 12:25) Kwa sababu hiyo, twapasa kupendezwa na mmoja na mwenzake na kuwa tayari kutoa usaidizi wenye upendo inapohitajiwa. Kielelezo kimoja ni kwamba, baadhi ya dada zetu wa kiroho miongoni mwetu wanalea watoto wao wakiwa peke yao katika kweli. Dada hawa wana daraka kubwa sana la kuzoeza watoto wao kiroho. Hakika wanastahili kitia-moyo chetu chenye fadhili na msaada “kulingana na mahitaji yao.” (Rom. 12:13a) Je, waweza kuwasaidia?

2 Njia Ambazo Waweza Kusaidia: Unapojitolea kuwapeleka mikutanoni kwa gari na kwenye mikusanyiko wale wanaotegemea usafiri wa umma unaweza kusaidia familia hiyo iokoe fedha nyingi. Kumsaidia mama kutunza watoto wadogo mikutanoni kwaweza kumfanya anufaike kikamili na programu. Vivyo hivyo, unapojitolea kumsaidia anapopeleka watoto wake katika utumishi wa shambani anaweza kuhisi amepunguziwa daraka zito. Kupendezwa kikweli na watoto, yaani kuwafanya wawe marafiki, kwaweza kuwavutia sana vijana wetu kwa njia ifaayo. Kualika familia ya mzazi mmoja kwenye funzo letu la familia pindi kwa pindi kutawainua kiroho.

3 Tumia Busara: Twapaswa kuwa waangalifu kutolazimisha kutoa msaada kwa yule asiyeuhitaji. Wala hatungetaka kuingilia mambo ya faragha ya familia ya mtu tunapotoa msaada unaohitajika. Bila shaka, akina dada na wenzi wa ndoa wangekuwa katika hali nzuri kusaidia dada anayehitaji msaada.

4 Wakristo wote wanatiwa moyo ‘kufuata mwendo wa ukaribishaji-wageni’ kuelekea mtu na mwenzake. (Rom. 12:13b) Kusaidia ndugu na dada zetu wa kiroho ni moja kati ya njia nyingi tunazoweza kuonyesha upendo wetu wa Kikristo tulio nao miongoni mwetu.—Yn. 13:35.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki