Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/00 uku. 8
  • Omba Msaada

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Omba Msaada
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Uangalizi Wenye Upendo Hujenga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Wazee Hulitumikia Kutaniko Jinsi Gani?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • “Lichungeni Kundi la Mungu Lililo Chini ya Uangalizi Wenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Wazee Wanaosimamia Vema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 3/00 uku. 8

Omba Msaada

1 Maneno haya yaliyopuliziwa “zilizo ngumu kushughulika nazo” hufafanua ifaavyo nyakati zetu zenye hatari. (2 Tim. 3:1) Kwa sababu hiyo, unaweza kufanya nini unapopatwa na magumu ya kiroho ambayo unahisi huwezi kukabiliana nayo?

2 Je, uko tayari kuongea na mshiriki aliyekomaa wa kutaniko? Huenda watu fulani wakasita kufanya hivyo kwa sababu ya kuona aibu, kutotaka kuwa mzigo kwa mtu yeyote, au kuwa na shaka kama mtu yeyote anaweza kusaidia. Kwa kweli, twapaswa kujitahidi kutunza madaraka yetu wenyewe kadiri tuwezavyo, lakini sikuzote twapaswa kujihisi huru kutafuta msaada katika mambo yanayohusu hali yetu ya kiroho.—Gal. 6:2, 5.

3 Mahali pa Kuanzia: Labda waweza kumwendea kiongozi wa funzo lenu la kitabu na umuulize kama unaweza kuhubiri naye katika utumishi wa shambani. Hiyo itakupatia fursa ya kumwambia juu ya tamaa yako ya kukua kiroho. Ikiwa yeye ni mtumishi wa huduma, mjulishe uhitaji wako wa msaada wa kiroho naye ataomba wazee wakusaidie. Au huenda ukamwendea mmoja wa wazee kuhusu mambo yanayokuhangaisha.

4 Wahitaji msaada wa aina gani? Je, kuna kitu ambacho kimefanya bidii yako ififie? Je, wewe ni mzazi aliye peke yake anayejaribu kusaidia watoto wawe karibu na kutaniko? Je, wewe ni mzee-mzee anayehitaji msaada? Au kuna tatizo fulani linalokusumbua? Kushughulika na siku zetu zenye hatari kwaweza kuwa jambo gumu—lakini ni jambo linalowezekana. Msaada upo.

5 Jinsi Ambavyo Wazee Husaidia: Wazee hujali kwelikweli. Watasikiliza mahangaiko yako. Wahubiri wengine wakipatwa na vizuizi kama hivyo, wazee watafikiria sana juu ya hilo wanapofanya ziara ya uchungaji na kufundisha kutaniko. Wakiwa “vielelezo kwa kundi,” wanadumu wakiwa tayari kufanya kazi nawe kwa shangwe. (1 Pet. 5:3) Kuwasikiliza ndugu hawa wanaposababu juu ya kanuni za Biblia kwaweza kuboresha huduma yako na kukusaidia katika maisha yako ya kibinafsi.—2 Tim. 3:16, 17.

6 Yesu ametupatia “zawadi [nyingi] zikiwa wanadamu.” (Efe. 4:8, kielezi-chini katika New World Translation of the Holy Scriptures—With References.) Hiyo yamaanisha kwamba wazee wako tayari kukutumikia. Wako ili kukusaidia na tuseme, ‘ni wako.’ (1 Kor. 3:21-23) Kwa hiyo badala ya kusitasita, sema waziwazi. Omba msaada unaohitaji.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki