Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/00 uku. 8
  • Kujifunza Kitabu Unabii wa Danieli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujifunza Kitabu Unabii wa Danieli
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Kitabu Cha Danieli Kinavyokuhusu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Yehova Amwahidi Danieli Thawabu ya Ajabu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Danieli Kitabu Kilichohakikishwa Kuwa cha Unabii
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Tutajifunza Kitabu Furaha ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 3/00 uku. 8

Kujifunza Kitabu Unabii wa Danieli

1 Kuanzia juma la Aprili 17, tutajifunza kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! katika Funzo la Kitabu la Kutaniko. Tayari wengi wamekisoma kitabu hiki chenye kusisimua, lakini sasa tuna fursa ya kufurahia manufaa zinazotokana na mazungumzo ya kikundi ya habari hiyo. Wahubiri wote, watu wenye kupendezwa, na watoto wanaalikwa, naam, wanatiwa moyo, kuwako kila juma kwa ajili ya funzo hilo lenye kina la kitabu cha Biblia cha Danieli.—Kum. 31:12, 13.

2 Ratiba ya Funzo na Maagizo: Ratiba kamili ya funzo la kitabu Unabii wa Danieli iko katika toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu. Hakikisha umeweka nakala yako kwenye kitabu chako cha funzo. Ratiba hiyo yaonyesha sura na mafungu kutoka katika kitabu hicho na pia mistari kutoka katika Danieli ambayo itazungumziwa katika sehemu ya kila juma. Vielezi-chini vyaeleza jinsi na wakati ambapo habari iliyo katika kitabu itakaposomwa. Katika umalizio wa funzo la kila juma, kiongozi anatiwa moyo kuzungumzia pamoja na kikundi mistari hususa kutoka katika Danieli iliyoorodheshwa kwenye ratiba ya juma hilo. Wakati ukiruhusu, mistari hiyo yaweza kusomwa na kuelezwa. Mistari kadhaa itaendelea kutoka juma moja hadi jingine kwa sababu ya mazungumzo yenye kuendelea ya matumizi yake.

3 Jitayarishe kwa Funzo Lenye Kina: Jitihada imefanywa ili kuruhusu wakati wa kutosha kila juma kwa mazungumzo yasiyo ya haraka ya mgawo wa habari hiyo. Masomo manne ni mafupi. Kwa sababu hiyo, mwishoni mwa funzo la juma la Juni 5, kiongozi aweza kutia ndani mazungumzo ya Danieli 2:1-40. Juma la Juni 26, aweza kuzungumzia Danieli 3:1-30. Juma la Septemba 4 lapaswa kutia ndani mazungumzo ya kina kirefu ya picha na maandiko yaliyo kwenye ukurasa wa 139. Chati iliyo kwenye ukurasa wa 188 na 189 yapaswa kuzungumziwa kwenye funzo la juma la Oktoba 2.

4 Jitayarishe vizuri kwa ajili ya funzo kila juma, na ufurahie kushiriki. Thamini pendeleo lako la kushirikiana na tengenezo la Yehova linaloonekana na kunufaika kutokana na ufahamu wenye kina na uelewevu ulioandaliwa na watiwa-mafuta waaminifu. (Dan. 12:3, 4) Tia moyo wengine kwa fadhili wahudhurie funzo la kitabu kwa ukawaida. Sisi sote na tukazie uangalifu neno la Mungu la kiunabii kama lifunuliwavyo katika kitabu cha Danieli chenye kutia kicho.—Ebr. 10:23-25; 2 Pet. 1:19.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki