Tutajifunza Kitabu Furaha ya Familia
Utaterema kujua kwamba kuanzia juma la Oktoba 6, 1997, tutachunguza kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko. Hakuna atakayetaka kukosa kuwapo kwenye funzo la kikundi la mwongozo huu wa Kimaandiko wenye kutumika kwa ajili ya maisha ya familia yenye furaha. Ratiba ya funzo itaruhusu uchunguzi kamili wa kila fungu na andiko la Biblia lililo katika kitabu hicho.
Sura yote ya kwanza itachunguzwa juma la kwanza la funzo, kwa kuwa ina maandiko machache yasiyonukuliwa. Kwa sababu hiyohiyo, sura ya 15 itachunguzwa katika kipindi kimoja. Hata hivyo, sura zote zitagawanywa katika sehemu mbili, karibu nusu ya sura itachunguzwa kila juma. Hivyo, kutakuwa na wakati wa kutosha kusoma na kuzungumzia maandiko yote yaliyotajwa bila kunukuliwa pamoja na kuchunguza kwa uangalifu matumizi ya maandiko yote yaliyonukuliwa katika kila fungu.
Sehemu ya maana ya funzo itakuwa mazungumzo ya habari katika sanduku la kufundisha kwenye umalizio wa kila sura. Kwa hiyo, wakati wa kutosha wapasa kutengwa ili kuchunguza maswali na maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa katika sanduku.
Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wanasihiwa waelekeze uangalifu wa pekee kwenye utayarishaji wao kwa ajili ya funzo na kuwatia moyo wote katika kikundi chao, kutia na wapya, watayarishe vizuri, wahudhurie kwa ukawaida, na washiriki.—om-SW 74-76.