Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/04 uku. 1
  • Sehemu ya 4: Kuwazoeza Wanafunzi Kujitayarisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sehemu ya 4: Kuwazoeza Wanafunzi Kujitayarisha
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Sehemu ya 2: Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Jitayarishe Vizuri Kufundisha
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 12/04 uku. 1

Sehemu ya 4: Kuwazoeza Wanafunzi Kujitayarisha

Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

1 Kwa kawaida, mwanafunzi anayejitayarisha mapema kwa ajili ya funzo, anayepiga mistari kwenye majibu, na anayefikiria jinsi ya kutoa majibu hayo katika maneno yake mwenyewe, atafanya maendeleo ya kiroho haraka. Kwa hiyo, unapoanzisha funzo, tayarisha somo fulani pamoja na mwanafunzi ili kumwonyesha jinsi ya kufanya hivyo. Kuhusiana na wanafunzi walio wengi, itafaa kutayarisha somo au sura nzima pamoja.

2 Kupiga Mistari na Kuandika Pambizoni: Mweleze jinsi ya kutafuta majibu ya maswali yaliyo kwenye kitabu. Mwonyeshe mwanafunzi nakala yako ya kichapo cha funzo ambacho umepiga mistari maneno au vifungu muhimu pekee. Mnapozungumzia habari hiyo, huenda mwanafunzi akataka kufuata kielelezo chako, kwa kupiga mistari maneno au vifungu muhimu katika nakala yake, ambavyo vitamsaidia kukumbuka jibu. (Luka 6:40) Kisha mwombe atoe jibu kwa maneno yake mwenyewe. Jambo hilo litakusaidia kujua kama mwanafunzi ameelewa vizuri habari mnayozungumzia.

3 Mwanafunzi anapojitayarisha kwa ajili ya funzo, ni muhimu achunguze kwa makini maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa. (Mdo. 17:11) Msaidie atambue kwamba kila andiko lililotajwa bila kunukuliwa linaunga mkono jambo fulani katika fungu. Mwonyeshe jinsi ya kuandika maelezo mafupi kuhusu maandiko pambizoni mwa kichapo cha funzo. Mweleze waziwazi kwamba Biblia ndiyo msingi wa yale anayojifunza. Mtie moyo atumie maandiko mengi iwezekanavyo anapotoa maelezo wakati wa funzo.

4 Kupitia Habari kwa Ufupi na Kurudia Mambo Makuu: Kabla ya mwanafunzi kuanza kutayarisha habari mtakayojifunza, itafaa aipitie kwa ufupi. Mtajie kwamba anaweza kufanya hivyo kwa kuchunguza kichwa kikuu cha habari, vichwa vidogo, na picha. Mweleze kwamba kabla hajamaliza kutayarisha, ingefaa arudie mambo makuu katika funzo, labda kwa kutumia sanduku la pitio ikiwa lipo. Kufanya hivyo kutamsaidia kukumbuka habari anayojifunza.

5 Kumzoeza mwanafunzi kutayarisha vizuri kwa ajili ya funzo lake kutamsaidia atoe maelezo yenye kujenga kwenye mikutano ya kutaniko. Pia kutamsaidia kusitawisha mazoea mazuri ya kujifunza hata baada ya kumaliza funzo lake la Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki