Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/04 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 13
  • Juma Linaloanza Desemba 20
  • Juma Linaloanza Desemba 27
  • Juma Linaloanza Januari 3
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 12/04 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Desemba 13

Wimbo 47

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Inapofaa, watie moyo wote watazame video No Blood—Medicine Meets the Challenge ili kujitayarisha kwa ajili ya mazungumzo ya juma lijalo. Taja mipango ya pekee ya utumishi wa shambani Desemba 25 na Januari 1. Ukitumia madokezo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa katika eneo lenu) panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 15 na Amkeni! la Novemba 22. Maonyesho mengine yanayofaa yanaweza kutumiwa. Katika kila onyesho, onyesha jinsi ya kushughulikia kizuia-mazungumzo “Tayari naijua sana kazi yenu.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, uku. wa 20.

Dak. 15: “Msaada Wako Unahitajiwa.”a Mhoji kwa ufupi mzee wa kutaniko. Mwombe aeleze kilichomsaidia astahili kuwa mzee na kilichomtia moyo ajitahidi kufikia pendeleo hilo la kutumikia kutanikoni.

Dak. 20: “Tunawezaje Kuwahubiria Watu wa Jamaa Zetu?”b Tumia maswali yaliyopo. Waombe wasikilizaji waeleze kwa ufupi jinsi ambavyo wameweza kuchochea upendezi na kuwahubiria watu wa ukoo.

Wimbo 17 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 20

Wimbo 68

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 15: “Jinsi Shule ya Huduma ya Kitheokrasi Inavyotunufaisha.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Tia ndani maelezo kutoka katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2004. Panga mapema ili mhubiri mmoja au wawili waeleze jinsi wanavyonufaika na shule hiyo.

Dak. 25: Zungumzia Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 1999, “Je, Uko Tayari kwa Hali ya Dharura?” Au mahali video inapopatikana uzungumzie, “Nufaika na Video No Blood—Medicine Meets the Challenge.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea video No Blood, ukitumia maswali kwenye ukurasa wa 6. Baadaye, soma fungu la mwisho. Watie moyo wote wawepo juma lijalo ili kuzungumzia maandalizi ya kutusaidia kuepuka kutiwa damu.

Wimbo 50 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 27

Wimbo 36

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za Desemba. Ukitumia madokezo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa katika eneo lenu), panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 1 na Amkeni! la Desemba 8.

Dak. 25: Kutii Amri ya Mungu ya Kujiepusha na Damu. Hotuba itolewe na mzee, akitumia hotuba ya kusomwa kutoka ofisi ya tawi. Mwanzoni, taja kwamba kadi za Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia hazipaswi kujazwa jioni hiyo. Anaposoma hotuba hiyo, msemaji anaweza kuongeza maelezo mafupi ili kukazia mambo makuu lakini hapaswi kutaja mifano wala maandiko zaidi. Maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa yanaweza kusomwa au kunukuliwa ikitegemea wakati. Unaposoma sehemu fulani za hotuba hiyo, kazia habari kwenye sanduku “Maandalizi ya Kutusaidia Tujiepushe na Damu.” Mwandishi anapaswa kuwapa wahubiri waliobatizwa kadi za Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia ikiwa wanahitaji kadi mpya. Mwandishi anapaswa pia kuhakikisha kwamba kuna Kadi za Utambulisho za kutosha.

Dak. 10: Daraka la Dhamiri Yako. Hotuba itolewe na mzee ikitegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 2004, ukurasa wa 23-24, fungu la 16-19. Kazia kwamba maamuzi tunayokabili kuhusiana na dhamiri ni mazito, kwa kuwa yanahusu uhusiano wetu na Yehova.

Wimbo 8 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 3

Wimbo 27

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Taja toleo la fasihi la Januari. Habari za Kitheokrasi na “Mambo Makuu Katika Ripoti ya Mwaka wa Utumishi wa 2004.”

Dak. 15: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu ya 4.” Baada ya utangulizi usiozidi dakika moja unaotegemea fungu la 1, panga kuwe na onyesho la dakika tano likitegemea fungu la 2-3. Katika onyesho hilo, kiongozi wa funzo la Biblia anamwonyesha mwanafunzi jinsi ya kujitayarisha kwa ajili ya funzo, akitumia fungu moja katika kitabu Ujuzi au broshua Anataka. Kisha zungumzia fungu la 2-5 kwa maswali na majibu, huku ukikazia mambo makuu katika onyesho hilo.

Dak. 15: “Makusanyiko ya Wilaya ya Mashahidi wa Yehova ya 2005 ya ‘Utii wa Kimungu.’”c Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Watie moyo wote wafanye mipango mapema iwezekanavyo ili wahudhurie kusanyiko.

Wimbo 79 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha endelea na mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki