Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/04 uku. 7
  • Mambo Makuu Katika Ripoti ya Mwaka wa Utumishi wa 2004

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mambo Makuu Katika Ripoti ya Mwaka wa Utumishi wa 2004
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 12/04 uku. 7

Mambo Makuu Katika Ripoti ya Mwaka wa Utumishi wa 2004

Burundi: Kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 5,459 mwezi wa Agosti. Wastani wa mafunzo ya Biblia 13,507 yaliongozwa kila mwezi. Watu 19,612 walihudhuria Ukumbusho. Habari njema zilihubiriwa katika maeneo mengi mapya wakati wa ile kampeni ya miezi mitatu ya kuhubiri katika maeneo ya mbali. Vikundi vitatu vilianzishwa huko Busoni, Mabayi, na Makamba. Burundi ilikuwa na ongezeko asilimia 11.

Eritrea: Licha ya hali ngumu wanayokabili, wahubiri katika nchi hiyo walitumia wastani wa saa 14.6 kila mwezi katika utumishi wa shambani, mapainia wasaidizi wakatumia wastani wa saa 55.7, nao mapainia wa kawaida wakatumia wastani wa saa 75.7. Watu 1,031 walihudhuria Ukumbusho. Eritrea ilikuwa na ongezeko la asilimia 2.

Kenya: Kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 19,314 mwezi wa Agosti. Kwa wastani, mafunzo ya Biblia 30,939 yaliongozwa kila mwezi, nao wastani wa mafunzo kwa kila mhubiri ulikuwa 1.1. Watu 1,450 walibatizwa mwaka huo. Ukumbusho ulihudhuriwa na watu 53,779. Kenya ilikuwa na ongezeko la asilimia 5.

Sudan: Katika mwaka huo wa utumishi, magazeti na broshua 46,014 ziliachiwa watu nchini Sudan. Watu 6,126 walihudhuria Ukumbusho, jambo linaloonyesha kwamba kutakuwa na ongezeko kubwa wakati ujao. Sudan ilikuwa na ongezeko la asilimia 4.

Tanzania: Tanzania ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 13,416 mwezi wa Agosti na ongezeko la asilimia 7. Katika mwaka wa utumishi wa 2004 mafunzo ya Biblia 20,462 yaliongozwa, nayo idadi ya makutaniko na vikundi ikaongezeka kutoka 361 hadi 401! Watu 51,323 walihudhuria Ukumbusho ikilinganishwa na watu 48,630 ambao walihudhuria mwaka uliotangulia. Bila shaka, kuna sababu nzuri za kutarajia kuwa na wahubiri wapya wengi mwaka huu.

Uganda: Kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 3,743 mwezi wa Agosti. Waliobatizwa mwaka wa utumishi wa 2004 walikuwa 358, ongezeko la asilimia 29 ikilinganishwa na waliobatizwa mwaka uliotangulia. Mafunzo ya Biblia zaidi ya 8,000 yanaongozwa kwa ukawaida kila mwezi! Watu 13,248 walihudhuria Ukumbusho. Idadi hiyo ni mara 3.5 zaidi ya kilele cha wahubiri cha mwaka huo wa utumishi. Nchi hiyo ilikuwa na ongezeko la asilimia 10.

Mambo hayo makuu yanaonyesha kwamba wahubiri wanaendelea kutii amri ya kiongozi wetu Yesu Kristo ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Mt. 24:14; 28: 19, 20) Yehova anabariki jitihada zetu na bila shaka tunamshukuru kwa kuharakisha kazi ya kuhubiri tunapokaribia mwisho wa mfumo huu wa mambo. (Isa. 60:22) Sasa tunatazamia kwa hamu utendaji wote wa kiroho uliopangwa kwa ajili ya mwaka wa utumishi wa 2005, na tunawatia moyo wahubiri wote waendelee kushiriki katika utumishi wa shambani kwa ukawaida.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki