Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 uku. 1
  • “Pigana Pigano Bora la Imani”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Pigana Pigano Bora la Imani”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Vile Vita vya Kufanya Yaliyo Mema
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Kutangaza Habari Njema—Katika Kutoa Ushuhuda Tukiwa Kikundi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 uku. 1

“Pigana Pigano Bora la Imani”

1 Mtume Paulo alimshauri Timotheo ‘apigane pigano bora la imani.’ (1 Tim. 6:12) Paulo mwenyewe aliishi kupatana na maneno hayo. Mwishoni mwa maisha yake, aliongea kwa uhakika kwamba yeye binafsi alikuwa amepigana pigano bora. (2 Tim. 4:6-8) Kwa kila njia, alitimiza huduma kwa ujasiri, moyo mkuu, na uvumilivu. Kwa kuiga kielelezo chake, twaweza kuwa na uhakika huohuo moyoni mwetu kwamba tunafanya yote tuwezayo katika pigano letu la imani ya Kikristo.

2 Tia Jitihada Inayohitajiwa: Paulo alijitahidi katika huduma. (1 Kor. 15:10) Sisi pia hujitahidi kutafuta watu wowote wanaostahili katika eneo letu. (Mt. 10:11) Ili kufikia baadhi yao, huenda ikatubidi kuamka mapema sana ili kuwahubiria wale tunaokutana nao barabarani. Au huenda ikatubidi kuhubiri hadi saa za jioni hivi ili kukutana na watu baada ya wao kurudi nyumbani mwao.

3 Twahitaji kujitia nidhamu na kuwa na ratiba nzuri ili kufika kwa wakati tunapokutana katika kikundi chetu cha funzo la kitabu kwa ajili ya utumishi wa shambani. Kwa mfano, baadhi ya washiriki wa familia ya Betheli husafiri kwa dakika 60 kwenda na kurudi siku za mwisho-juma ili kushiriki katika huduma pamoja na makutaniko yao waliyogawiwa. Pia, huenda tukawathamini wahubiri fulani na familia zilizo katika kutaniko letu ambazo husafiri mwendo mrefu lakini hufika kwa wakati. Vielelezo hivyo vya bidii na utaratibu mzuri wa kibinafsi vyastahili kuigwa.

4 Twapasa kuchochewa kufuatia watu wote waliopendezwa ambao tumewapata. Hata tunapoangusha vichapo barabarani au tutoapo ushahidi wa vivi hivi, twahitaji kujitahidi kuchukua anwani au namba ya simu ya mtu huyo. Kisha tunaweza kumrudia ili kuendeleza upendezi wake na kujitahidi kuanzisha funzo la Biblia.

5 Uwe wa Kawaida Katika Utumishi: Paulo alidumu katika huduma yake, akiifanya kikamili. (Rom. 15:19) Vipi wewe? Je, wewe hushiriki katika huduma kwa ukawaida? Je, tayari umeenda katika utumishi wa shambani mwezi huu? Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wanapendezwa kuona kwamba kila mtu katika kikundi chao anashiriki katika huduma mwezi wa Agosti. Watakusaidia ufanye hivyo.

6 Kwa kuiga kielelezo cha Paulo katika kutegemeza habari njema kikamili, tutaendelea ‘kupigana pigano bora la imani.’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki