Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 uku. 1
  • Je, Unavumilia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unavumilia?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Wewe Utaendelea Kutembea Katika Ukweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • “Mfikirieni Sana Yeye Ambaye Amevumilia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
  • Uvumilivu—Muhimu kwa Wakristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • “Acheni Uvumilivu Ukamilishe Kazi Yake”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 uku. 1

Je, Unavumilia?

1 “Sina kisababishi cha shukrani kilicho kikubwa zaidi kuliko mambo haya, . . . kwamba watoto wangu waendelea kutembea katika kweli.” (3 Yoh. 4) Uvumilivu wa watoto wa kiroho wa Yohana ulimletea shangwe kuu. Jinsi inavyomfurahisha Baba yetu wa kimbingu kuona mamilioni ya wale wanaotazamiwa kuwa watoto wake “waendelea kutembea katika kweli”!—Mit. 23:15, 16; 27:11.

2 Ijapokuwa kwa ujumla watu wa Mungu wanaendelea na utendaji wa Kikristo wenye bidii, wengine wamepunguza mwendo. Ingawa huenda watu hao walikuwa na bidii mwanzoni walipojifunza kweli, miaka ilipopita, wametosheka na kushiriki mara chache tu katika kazi ya kufanya wanafunzi.

3 Ni jambo linaloeleweka kwamba huenda wengine wakapunguza mwendo kwa sababu ya kudhoofika kwa afya na athari za uzee. Hata hivyo, wanapaswa kupongezwa kwa uvumilivu wao. Wanafanya yale wawezayo. Lakini kila mtu aliyeweka maisha yake wakfu kwa Mungu apaswa kujiuliza hivi: ‘Je, nimejiruhusu nikazie fikira mambo yangu ya kibinafsi hivi kwamba masilahi ya Ufalme hayana sehemu kubwa maishani mwangu? Je, nimekuwa “vuguvugu,” au ningali najikakamua “kisulubu”?’ (Ufu. 3:15, 16; Luka 13:24) Sisi sote na tufikirie kwa sala kile tunachofanya na kufanya maendeleo yanayohitajika, tukikumbuka kwamba Yehova anaahidi kuandaa “utukufu na heshima na amani kwa kila mtu afanyaye lililo jema.”—Rom. 2:10.

4 Jinsi ya Kuvumilia: Ni nini kilichomsaidia Yesu kuvumilia? Paulo alieleza: “Kwa ajili ya shangwe iliyowekwa mbele yake alivumilia mti wa mateso, akidharau aibu, na ameketi kwenye mkono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Mungu.” (Ebr. 12:1-3) Shangwe iliyowekwa mbele ya Yesu ilishinda sana majaribu yaliyokuwa ya muda mfupi tu ambayo ilimbidi akabiliane nayo. Kukumbuka shangwe ambayo imewekwa mbele yetu kwaweza kutusaidia tuvumilie pia. (Ufu. 21:4, 7; 22:12) Tukimtegemea Yehova atupe nguvu kupitia funzo la kibinafsi, kuhudhuria mikutano kwa ukawaida, na kudumu katika sala, tutaweza kuvumilia katika kazi aliyotupa kufanya.

5 Yehova hufurahia uvumilivu wa washikamanifu wake. Kwa hiyo na tuongeze shangwe yake kwa kuendelea “kutembea katika kweli.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki