Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Agosti 14
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Taja ripoti ya utumishi wa shambani ya Aprili ya nchi na ya kutaniko la kwenu. Ni miisho-juma miwili tu iliyobaki Agosti, kwa hiyo tia moyo kila mtu ashiriki katika huduma kabla ya mwezi kwisha. Zungumzia ratiba ya mwisho-juma ya mikutano ya utumishi wa shambani.
Dak. 15: “Pigana Pigano Bora la Imani.” Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatie kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Toa maelezo ya ziada kutoka katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 43-45, juu ya jinsi ambavyo viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko hupanga utendaji wa utumishi wa shambani wa vikundi vyao na kumsaidia yeyote anayehitaji msaada wa kibinafsi ili ashiriki katika huduma na kutoa ripoti kwa ukawaida.
Dak. 18: Jinsi Unavyoweza Kunufaika Unapoenda Shuleni. Baba aongea na watoto wake akiwasaidia wathamini kwa nini elimu ya kilimwengu ni yenye manufaa. (Ona kitabu Vijana Huuliza, ukurasa wa 133-139.) Vijana wengi huhisi kwamba kwenda shule ni jambo gumu sana katika jamii ya siku hizi yenye ukaidi. Pia wao huhisi wamechoshwa, wakikata kauli kwamba yale wanayojifunza hayatawasaidia sana. Baba azungumzia kanuni za Kimaandiko na sababu zifaazo zinazoonyesha hekima ya kupata elimu ya kutosha ya kilimwengu. Awatia moyo watoto wake wajifunze vizuri na kusikiliza kwa makini darasani.
Wimbo 127 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 21
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Panga kuwe na wonyesho wa utumishi wa shambani uliofanyiwa mazoezi vizuri kuonyesha jinsi ya kujibu swali hili: “Sababu gani Mungu wa upendo angeruhusu kuteseka kuendelee muda mrefu Sana?” (Kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 134) Tia moyo kila mtu ashiriki katika huduma mwisho-juma huu.
Dak. 8: “Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee.” Hotuba. Tangaza tarehe ya kusanyiko la pekee lifuatalo, kama yajulikana, na usihi wote wahudhurie siku yote. Tia moyo wahubiri waalike watu wenye kupendezwa na mafunzo ya Biblia.
Dak. 25: “Je, Wajinufaisha?” Maswali na majibu.
Wimbo 152 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Agosti. Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wapaswa kuuliza kila mtu katika kikundi chao ili ripoti zote zihesabiwe kufikia Septemba 6.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: “Mikutano Hunufaisha Vijana.” Mazungumzo ya maswali na majibu yakiongozwa na mzee. Unapozungumzia fungu la 8, fikiria mambo fulani yafaayo ambayo huchochea kukazia fikira na kusikiliza kwa makini wakati wa mikutano. (Ona Amkeni!, Septemba 22, 1998, ukurasa wa 19-20.) Tia moyo wazazi wasisitize kwamba watoto wao wahudhurie mikutano yote kwa ukawaida.—Ona jambo lililoonwa katika Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 1997, ukurasa wa 25.
Wimbo 176 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 4
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Sanduku la Swali. Panga wahubiri wasimulie mambo yaliyoonwa walipokuwa wakitoa ushahidi wa vivi hivi wakienda kwenye mkusanyiko wa wilaya, wakiwa huko, au wakirudi kutoka huko.
Dak. 10: Wakati Wetu Ni wa Pekee. Hotuba itolewe na mzee, ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Novemba 15, 1996, ukurasa wa 22-23.
Dak. 20: “Je, Unavumilia?” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia moyo wote wafikirie jinsi walivyofanikiwa kuvumilia katika huduma ya Kikristo. Udhaifu ukionekana, kuna uhitaji wa kujiimarisha kiroho. Tia ndani maelezo kutoka katika Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 1999, ukurasa wa 20-21, fungu la 17-21. Omba wahubiri wawili au watatu ambao wamevumilia kwa uaminifu kwa kipindi cha miaka kadhaa wasimulie kile kinachowasaidia wavumilie.
Wimbo 206 na sala ya kumalizia.