Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/02 kur. 3-4
  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Lihubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • ‘Fanyeni Lililo Jema Kuelekea Wote’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 3/02 kur. 3-4

‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’

1 Mtume Paulo alifanya kazi kwa ukaribu pamoja na Timotheo na Tito katika miaka ya mwisho ya huduma yake aliyoifanya kwa bidii. Aliwaandikia wote wawili maneno yanayofanana ya kuwatia moyo. Alimwambia Tito kwamba “wale ambao wameamini Mungu” wanapaswa “kuweka akili zao juu ya kudumisha kazi zilizo bora.” (Tito 3:8) Alimwambia Timotheo kwamba wale ambao wameweka tumaini lao kwa Mungu wanapaswa “kuwa matajiri katika kazi zilizo bora.” (1 Tim. 6:17, 18) Hilo ni shauri bora kwetu sote! Lakini ni nini kitakachotuchochea tufanye kazi zilizo bora? Na ni kazi gani hususa ambazo twaweza kufanya katika siku zijazo?

2 Imani na upendo wetu kwa Yehova pamoja na tumaini ambalo ametupatia, hutuchochea kuwa matajiri katika kazi zinazofaa. (1 Tim. 6:19; Tito 2:11) Hasa wakati huu wa mwaka, twakumbushwa kwamba Yehova alimtuma Mwana wake Yesu duniani ili kumwondolea lawama Baba yake na kutayarisha njia ya uhai kwa wanadamu wote wanaostahili. (Mt. 20:28; Yn. 3:16) Jambo hilo litaonyeshwa wazi kwenye mwadhimisho wa Ukumbusho wa kifo cha Kristo mnamo Machi 28. Ili tuonyeshe kwamba twathamini tumaini letu la kupata uhai udumuo milele, je, hatuchochewi kufanya yote tuwezayo “kuwa matajiri katika kazi zilizo bora”? Bila shaka! Ni kazi gani ambazo twaweza kufanya sasa?

3 Kufanya Kazi Zilizo Bora Katika Machi na Kuendelea: Kwa hakika, tutahudhuria Ukumbusho—tukio muhimu zaidi mwaka huu kwa Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. (Luka 22:19) Lakini twataka kuwaalika watu wengi iwezekanavyo wafurahie pindi hiyo pamoja nasi. Tazama ripoti ya utumishi katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 2002, nawe utaona kwamba mwaka uliopita, hudhurio la Ukumbusho katika nchi nyingi duniani lilizidi idadi ya wahubiri kwa mara tatu, nne, tano, au hata zaidi. Kwa kweli, wote katika makutaniko hayo walijitahidi sana kugawanya mialiko ya Ukumbusho kotekote katika eneo lao. Kwa hiyo, twataka kutumia wakati mwingi sana tuwezavyo kati ya sasa na Machi 28 kualika watu kwenye Ukumbusho, tukiwasaidia wajifunze kuhusu tumaini la wokovu.

4 Twaweza kuonyeshaje kwamba sisi ni “matajiri katika kazi zilizo bora” wakati wa majira haya ya Ukumbusho? Kwa kuendelea kushiriki katika kazi ya kuhubiri habari njema kwa uchangamfu, kuwa “wenye bidii kwa kazi zilizo bora.” (Tito 2:14; Mt. 24:14) Ikiwa hukuweza kufanya upainia msaidizi mwezi wa Machi, je, waweza kufanya hivyo mwezi wa Aprili/au Mei? Ikiwa unafanya upainia mwezi huu, je, waweza kuendelea?

5 Watu wengine wanaofanya kazi ya kimwili wameona kwamba wanaweza kutumia muda wa saa moja au zaidi katika utumishi wanapokwenda kazini, kwa kuwahubiria watu barabarani au kwa kuwahubiria wale ambao huanza biashara zao asubuhi na mapema. Wengine wamepanga kuhubiri saa za chakula cha mchana. Wengine wameweza kuongoza funzo la Biblia na mfanyakazi mwenzao katika kipindi hicho. Akina dada wengi ambao hawajaajiriwa wameweza kutenga wakati kwa ajili ya huduma ya shambani watoto wao wanapokuwa shuleni. Kwa kuamka mapema kidogo siku fulani ili kufanya kazi zao za nyumbani, wamepata nafasi ya kuhubiri na kufundisha wakati wa mchana.—Efe. 5:15, 16.

6 Hata kama huwezi kufanya upainia-msaidizi, huenda unaweza kupanga kushiriki zaidi katika huduma, ukifanya yote uwezayo ‘kufanya mema, kuwa tajiri katika kazi zilizo bora, kuwa mkarimu, tayari kushiriki’ ukweli pamoja na wengine.—1 Tim. 6:18.

7 Kumbuka Kazi Bora ya Kufanya Wanafunzi: Kila mwaka watu wenye kupendezwa huja kwenye Ukumbusho. Je, inawezekana wengine katika kutaniko washughulikie wale wanaohudhuria ambao kwa sasa hawajifunzi? Je, wanaweza kurudiwa ili wasaidiwe kufanya maendeleo ya kiroho? Huenda ikawa kwamba baadhi ya wanaohudhuria Ukumbusho ni watu wa ukoo wa Mashahidi. Huenda ikawa wengine ni watu ambao walijifunza zamani na wanahitaji tu kutiwa moyo warudie funzo lao na kuhudhuria mikutano kwa ukawaida. Tutafurahi kama nini kuwaona wakiwa watumishi wa Yehova watendaji pamoja nasi!

8 Tukiongeza utendaji wetu katika huduma mwezi wa Machi na kuendelea, yaelekea kwamba tutapata watu wengi wenye kupendezwa ambao tutawarudia. Jaribu kuwaacha na swali fulani. Kisha waambie utalijibu utakaporudi. Tukifanya hivyo, tutakuwa tukitayarisha njia ya kufanya ziara ya kurudia. Itafaa turudi pasipo kukawia. Ikiwa hatukufaulu kuanzisha funzo katika ziara ya kwanza, twataka kujaribu kulianzisha katika ziara inayofuata ikiwezekana.

9 Tunapohubiri barabarani, twapaswa kujaribu kuanzisha mazungumzo na watu. Wahubiri wengi wamepewa majina, anwani, na namba za simu za watu wenye kupendezwa ambao walikutana nao walipokuwa wakihubiri barabarani. Ikiwa unakutana na mtu asiyeishi katika eneo lenu, chukua fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43-SW) kutoka kwenye Jumba la Ufalme, uijaze, na kumpa mwandishi wa kutaniko, ambaye ataituma kwenye kutaniko ambalo liko katika eneo la mtu huyo. Ikiwa mwandishi hawezi kufanya hivyo, ataituma kwenye ofisi ya tawi ishughulikiwe. Kwa njia hiyo, mtu fulani ataweza kufuatia upendezi.

10 Ikiwa umepewa namba ya simu ya mtu huyo, mrudie kwa kumpigia simu. Tayarisha mapema yale unayotaka kuzungumzia. Weka kitabu Kutoa Sababu karibu ili ukirejezee kwa uharaka. Akionyesha kupendezwa, mwambie akueleze mahali anapoishi ili umtembelee nyumbani ikiwezekana.

11 Shirikiana na Wazee Kusaidia Wasiotenda: Wazee wangependa sana kuhangaikia wasiotenda kwa upendo. Wengi wao tayari wameanza kuhudhuria mikutano tena bila kuchochewa na mtu yeyote. Wametambua uhitaji wa kushirikiana kwa ukaribu na tengenezo la Yehova ili wawe na usalama wa kiroho unaoelezwa katika Zaburi 91. Baadhi yao sasa wako tayari kushiriki katika utumishi wa shambani tena. Ikiwa kuna wasiotenda ambao watahudhuria Ukumbusho mwezi huu, huenda wakakubali kujifunza Biblia. Ikitukia hivyo, wazee watafanya mipango ili mtu fulani ajifunze na wale wanaohitaji msaada. Ukiombwa usaidie, jitihada zako zitathaminiwa na wazee.—Rom. 15:1, 2.

12 Endeleeni “Kudumisha Kazi Zilizo Bora”: Wengi ambao wamefanya upainia-msaidizi kwa mwezi mmoja au zaidi wameona kwamba utumishi wao wa shambani umeongezeka katika miezi inayofuata. Walikutana na watu wenye kupendezwa na wakawarudia. Hiyo iliwachochea wajitahidi kwenda katika utumishi wa shambani mara nyingi ili kuwatembelea tena watu hao wenye kupendezwa. Wengine walianzisha mafunzo ya Biblia, na hilo liliwasaidia kushiriki zaidi katika huduma.

13 Na wengine wamepata shangwe nyingi kwa kufanya mengi zaidi katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi hivi kwamba walichochewa kuchunguza mambo wanayopaswa kutanguliza. Tokeo ni kwamba, wengine waliweza kupunguza muda wanaotumia katika kazi ya kimwili na kuendelea kuwa mapainia-wasaidizi. Wengine wameanza utumishi wa painia wa kawaida. Hawakutumaini vitu vya ulimwengu huu, bali walimtumaini Mungu kabisa. Waliona kwamba kuwa “wakarimu, tayari kushiriki,” kuliwaletea baraka tele kutoka kwa Yehova na kuliimarisha tumaini lao la kufurahia “uhai ulio halisi.” (1 Tim. 6:18, 19) Bila shaka, wengi wafanyapo upainia, kutaniko zima hunufaika. Mapainia hupenda kuongea juu ya mambo yaliyoonwa na kualika wengine washiriki katika huduma pamoja nao, na hiyo huchochea hali nzuri ya kiroho katika kutaniko.

14 Sote na tuwe “matajiri katika kazi zilizo bora” katika majira haya ya Ukumbusho na kuendelea kwa kuongeza utendaji wetu katika huduma ya Kikristo. Na tuonyeshe kwamba twamshukuru Yehova kwa yale ambayo ametufanyia kwa kutupatia tumaini la kuishi milele katika dunia mpya yenye uadilifu.—2 Pet. 3:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki