Na Uwe Mtendaji Mwenye Furaha
1 Yesu alisema kwamba wakati wa kuwapo kwake, watu walio wengi zaidi ‘hawangejali,’ kama vile tu ilivyokuwa katika siku za Noa. (Mt. 24:37-39) Basi, yatazamiwa kwamba watu wengi hawatasikiliza habari njema za Ufalme. Ni nini kinachoweza kutusaidia tudumishe roho ya shangwe tunapotimiza huduma yetu?—Zab. 100:2.
2 Kwanza, twahitaji kukumbuka kwamba ujumbe wetu na utume wetu wa kuhubiri watoka kwa Mungu. Watu wasiposikiliza tunapowahubiria, zijapokuwa jitihada zetu bora, kwa kweli huwa wanamkataa Yehova. Kukumbuka kwamba uaminifu wetu katika kuhubiri unampendeza Yehova kutatusaidia tudumishe shangwe na furaha ya moyoni tukiwa watendaji wa neno ya Mungu.—Yak. 1:25.
3 Jambo la pili ni kwamba, kungali na watu ambao watakubali njia ya Yehova ya wokovu. Ingawa huenda wengi wakakataa, kungali na watu walio mfano wa kondoo ambao wanahitaji kukusanywa, hata sasa, siku hizi za mwisho kabisa. Twahitaji kuendelea kuhubiri, tukienda “katika jiji lolote lile au kijiji chochote kile” ‘tukitafuta kabisa ni nani humo anayestahili.’—Mt. 10:11-13.
4 Dumisheni Mtazamo Unaofaa: Hali ya kusikitisha ya dini bandia imewavunja moyo watu fulani. Wengine ‘wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku’ na mfumo huu wa mambo. (Mt. 9:36) Huenda wengi wakalemewa na ukosefu wa kazi, afya mbaya, na ukosefu wa usalama. Kuelewa hayo kutatusaidia twendelee na kazi yetu. Jitahidi kuanzisha mazungumzo yanayoshughulikia masuala yanayowahangaisha sana watu katika eneo letu. Wasaidie waone kuwa Ufalme wa Mungu ndio suluhisho pekee. Tumia Maandiko na mambo hususa katika vichapo ili kufikia mioyo yao na habari njema.—Ebr. 4:12.
5 Watendaji wenye furaha wa neno ya Mungu sikuzote hukumbuka hivi: “Furaha ya BWANA ni nguvu [yetu].” (Neh. 8:10) Hakuna haja ya kupoteza shangwe yetu. “Ikiwa hiyo nyumba inastahili, acheni amani mwitakiayo ije juu yayo; lakini ikiwa haistahili, acheni amani itokayo kwenu irudi juu yenu.” (Mt. 10:13) Yehova huongeza shangwe yetu na nguvu zetu tuvumiliapo kwa subira katika utumishi wake mtakatifu, naye hubariki uaminifu wetu.