Sanduku La Swali
◼ Kwa nini kuna uhitaji wa kuwa waangalifu tunapohubiri kupitia barua?
Kuhubiri kupitia barua kumekuwa njia yenye matokeo sana ya kujulisha wengine habari njema. Hata hivyo, matukio ya ulimwengu yamefanya watu watahadhari kufungua barua wasizojua. Bahasha kutoka mahali wasipojua au ambazo hazina anwani ya mahali zilipotoka mara nyingi huogopwa, hasa kama zimeandikwa kwa mkono na kama barua zenyewe ni kubwa. Huenda wenye nyumba wakatupa barua hizo bila kuzifungua. Twaweza kuzuiaje jambo hilo?
Ikiwezekana, tumia mashine ya kupiga chapa kuandika barua na kwenye bahasha pia. Bahasha yapaswa kuandikwa jina la mwenye nyumba. Usiandike “Kwa Mwenye Nyumba.” Kwa kuongezea, sikuzote andika anwani yako juu ya bahasha. Ikiwa haifai kuonyesha anwani yako, tumia jina lako na anwani ya Jumba la Ufalme. Usitume barua bila kujitambulisha. Usitumie kamwe anwani ya ofisi ya tawi.—Ona Sanduku la Swali la Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1996.
Madokezo zaidi na barua ya mfano yaweza kupatikana katika kitabu Faidika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ukurasa wa 71-73. Miongozo hii itatusaidia kutumia barua kwa matokeo tunapowahubiria wengine habari njema.