Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Je, wafikiri matatizo kama haya yatakwisha kweli? [Soma nukuu la kwanza lililo katika makala ya kwanza, na ungoje jibu.] Neno la Mungu lililopuliziwa hutuhakikishia kwamba matatizo hayo yatakwisha hivi karibuni. [Soma Zaburi 72:12-14.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi laeleza jinsi jambo hilo litakavyotimizwa.”
Amkeni! Juni 22
“Je, wafikiri kila mtu atafurahia uhuru wa kweli hapa duniani? [Ngoja jibu.] Ona ahadi hii yenye kupendeza ya Mungu. [Soma Waroma 8:21.] Ili ahadi hiyo itimie, lazima utumwa wote uishe, sivyo? Gazeti hili la Amkeni! laonyesha jinsi jambo hilo litakavyowezekana.”
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Mamilioni ya watu hutumia sanamu katika ibada yao, huku mamilioni ya watu wengine wakifikiri kwamba ni makosa kufanya hivyo. Je, umepata kujiuliza Mungu anaonaje jambo hilo? [Ngoja jibu. Kisha usome Yohana 4:24.] Makala hizi zaonyesha jinsi ibada ya sanamu ilivyoanza na kile ambacho Biblia husema kuhusu ibada hiyo.”
Amkeni! Julai 8
“Biblia ilitabiri kwamba siku za mwisho zingekuwa nyakati zilizo ngumu. [Soma 2 Timotheo 3:1, 3.] Ulimwenguni pote, ongezeko la uhalifu lathibitisha jambo hilo. Hali ingekuwa mbaya kama nini kama hakungekuwa na polisi! Gazeti hili la Amkeni! lazungumzia magumu ambayo polisi hukabili ulimwenguni pote.”