Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Feb. 15
“Watu fulani hujiuliza kama kuna Mungu mwenye utu. Watu wengine husema kwamba yeye yuko lakini wanaonelea kwamba yuko mbali nao. Je, umetambua jambo hilo? [Ngoja jibu.] Tafadhali ona vile kupata kumjua Mungu kibinafsi ni jambo muhimu sana. [Soma Yohana 17:3.] Kuhusiana na jambo hilo, utafurahia kusoma makala za kwanza za gazeti hili.”
Amkeni! Feb. 22
“Je, unafikiri Mungu alikusudia wanadamu, kutia na watoto, wapatwe na utapiamlo? [Ngoja jibu.] Ona ahadi hii yenye kufariji inayopatikana katika Biblia. [Soma Zaburi 72:16.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia visababishi vya utapiamlo na, la maana zaidi, ahadi ya Mungu ya kuukomesha hivi punde.”
Mnara wa Mlinzi Mac. 15
“Tungependa kujua maoni yako kuhusu andiko hili. [Soma Mathayo 5:10.] Mtu anawezaje kuwa na furaha anapoteswa? [Ngoja jibu.] Makala mbili za kwanza katika gazeti hili zinazungumza kuhusu watu fulani ambao waliendelea kuwa na furaha licha ya mateso. Utafurahi kusoma jinsi walivyofaulu.”
Amkeni! Mac. 8
“Je, hukubali kwamba licha ya matatizo tuliyo nayo maishani tuna sababu za kuwa wenye shukrani? [Ngoja jibu.] Jinsi ambavyo tumeumbwa ni sababu moja ya kuwa wenye shukrani. [Soma Zaburi 139:14.] Tunashukuru sana kwamba tuna hisi ambazo zinatuwezesha kufurahia maisha, kama vile toleo hili la Amkeni! linavyosimulia.”