Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
“Unafikiri familia zingekuwaje ikiwa zingefuata shauri hili? [Soma Waefeso 4:31. Kisha mruhusu ajibu.] Makala hii inatoa mapendekezo yanayofaa kutoka katika Biblia kuhusu kutatua matatizo na kudumisha furaha katika ndoa.” Zungumzia makala iliyo kwenye ukurasa wa 18.
Amkeni! Feb.
“Watu fulani wanaamini kwamba Mungu anarekodi kila kosa tunalofanya. Wengine wanafikiri kwamba anasamehe dhambi zote, hata ziwe nzito kadiri gani. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Matendo 3:19.] Makala hii inazungumzia hatua tatu zinazotajwa katika Biblia ambazo mtu anahitaji kuchukua ili aonyeshwe rehema na Mungu.” Zungumzia makala iliyo kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi Mac. 1
“Ningependa kupata maoni yako kuhusu andiko hili linalojulikana sana. [Soma Yohana 3:16.] Je, umewahi kujiuliza kifo cha mtu mmoja kingewezaje kuwaletea wengine uzima wa milele? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linatoa maelezo yaliyo wazi na yenye kuridhisha kuhusu jinsi tunavyoweza kunufaika kutokana na kifo cha Yesu.”
Amkeni! Mac.
“Je, unafikiri dini zote ni nzuri? [Mruhusu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema kuhusu ibada ya watu fulani. [Soma Marko 7:7.] Mtu anaweza kujuaje ikiwa dini inafundisha kweli wala si ‘amri za wanadamu’? Je, kweli ya kidini inaweza kupatikana? Gazeti hili linajibu maswali hayo.”